• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Wednesday, April 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Dkt. Kalemani awaonya wakandarasi umeme wa REA

by BAJETI
August 3, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI imewaonya  wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini kuwa haitaongeza muda kwa yeyote atakayechelewa kukamilisha ndani ya muda uliopangwa kwa mujibu wa mkataba.

Onyo hilo limetolewa na Waziri wa Nishati Dkt.Merdad Kalemani  wakati akizindua Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, katika Kijiji cha Matiri wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.

Amesema asilimia 10  ya malipo kwa mkandarasi yatakakwa kwa kuchelewesha kazi husika.

Hata hivyo Dkt.Kalemani ameongeza kuwa ni marufuku kwa wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika maeneo yote nchini kuacha tabia ya kuhamisha nguzo za umeme zilizosimikwa

Ameeleza kuwa, mkandarasi yeyote aliyesimika nguzo, haruhusiwi kuondoa nguzo hizo na kupeleka sehemu nyingine badala yake ahakikishe anasambaza umeme katika eneo hilo na kuunga wateja wa eneo hilo

Aidha amebainisha kuwa wananchi wanafahamu serikali imetoa fedha nyingi kuhakikisha vijiji vyote vinapata umeme bila kurukwa.

“Sitaki kuona mkandarasi anafikisha nguzo ‘Site’ anazisimika, au mwingine amezirundika hapo baada ya muda anazitoa wakati hapo hakuna umeme anapeleka sehemu nyingine ni marufuku, huku ni kugombanisha serikali na wananchi wake”amesema Dkt.Kalemani

Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Matiri wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani(hayupo pichani) wakati akizindua Mradi wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, wilayani Mbinga mkoani Ruvuma (Picha na Wizara ya Nishati)

Akizungumzia Usambazaji wa Umeme katika Wilaya ya Mbinga, Dkt. Kalemani amebainisha kuwa wilaya hiyo inajumla ya Vijiji 169, kati ya hivyo 71 vimepatiwa umeme na 98 vitapatiwa umeme katika mradi huo wa REA III mzunguko wa pili kwa gharama ya Sh.Bilioni 14.34.

Mkoa wa Ruvuma una jumla ya Vijiji  554 ambapo vijiji  289 tayari vimepata umeme  na 265 bado havijafikiwa katika Wilaya za Songea , Mbinga, Nyasa,Tunduru na Namtumbo ambapo zitatumika kiasi cha Sh.Bilioni 71.95 kwa mkoa mzima kukamilisha.

Next Post

Majimbo 35 yakumbwa na moto unaosababishwa na ongezeko la joto Uturuki

Afungwa maisha kwa kumlawiti mtoto wa miaka tisa

TAG yawataka waumini kuongeza maombi ili kuleta umoja katika jamii

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:12
  • Today's page views 19
  • Total visitors 15,847
  • Total page views 17,967

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In