MCHUNGAJI Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assembles of God Lazaro Mgimwa amewataka waumini wa Kanisa hilo wawajibike kwa nguvu kuongeza maombi na kumhubiri Yesu Kristo ili Kanisa la Mungu lisimame kwa kuleta umoja na upendo.
Hayo ameyasema leo Kigezi Buyuni jijini Ilala Mkoa wa Dar es Salaam wakati akifungua semina ya siku moja iliyofanyika kanisani hapo.
Mchugaji Mgimwa amesema kuwa semina hiyo itawasaidia waumini kusimama kwenye neno na kujiamini kwani Kanisa la sasa linahitaji uamsho wa maombi ili lisimame.
Amesema licha ya Kanisa kuhitaji uamsho wa maombi ili lisimame lakini pia uamsho huo usaidie katika kuleta umoja na upendo baina ya watanzania wote kupitia maombi.
“Hakuna kitu kinachohitajika kwa Kanisa kama uamsho wa maombi ya nguvu ya kumhubiri Yesu Kristo kwani baadhi ya wakristo ndani ya makanisa wekuwa wakilala na kujisahau wakati Mchungaji anatoa neno la Mungu.
“Baadhi ya waumini wakiingia katika ibada huwa wanapatwa na misongo ya mawazo na neno likianza tu kuhubiriwa wanapatwa na usingizi na mchungaji akihubiri neno haliwanufaishi wakristo wa namna hii”amesema Mchungaji Mgimwa.
Hata hivyo Mchungaji Mgimwa amelipongeza Kanisa la TAG kuadhimisha miaka 13 ya uamsho.
Discussion about this post