SEOUL,Korea Kusini
KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema dunia inahitaji ushirikiano wa kimataifa kushinda janga la ugonjwa wa Corona ili kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza kupitia ujumbe wa video katika ufunguzi wa mkutano wa ushirikiano wa kimataifa wa mwaka 2021 wa P4G unaofanyika mjini Seoul chini Jamhuri ya Korea Kusini amesema ikiwa serikali zitaafikiana kwa pamoja malengo ya kumaliza makaa ya mawe, kuongeza ahadi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuwekeza katika malengo ya dunia, kuna fursa ya kuishinda mabadiliko ya tabiachi.
Amesema dunia inahitaji ushirikiano wa kimataifa kushinda janga la Corona kufikia Malengo ya maendeleo ya maendeleo endelevu na kushughulikia mabadiliko ya tabianchi.
Mkutano huo wa ushirikiano wa ukuaji unaojali mazingira na malengo ya Ulimwengu 2030 (P4G) unakusudia kukuza ushirikiano wa soko na kuchagiza hatua za ngazi ya juu za kisiasa na sekta binafsi na umewajumuisha pamoja wakuu wa nchi, wakurugenzi watendaji na viongozi wa asasi za kiraia karibu na ajenda ya pamoja ya kuhamasisha uwekezaji kwa ajili ya mabadiliko yanayoonekana.
Akizungumzia kuhusu hewa ukaa, Guterres ameelezea kwamba ingawa kuna ahadi za kufanikisha kutozalisha kabisa hewa ukaa ifikapo 2050, bado kuna mengi ya kufanya ili kuziba pengo la uzalishaji wa hewa ukaa na kufikia malengo ya SDGs.”
Amesisitiza wito wake kwa wafadhili wote kuwasilisha michango mipya waliyoamua Kitaifa, kujitolea kutozalisha kabisa hewa ukaa ifikapo mwaka 2050 na muhimu zaidi wa kuweka sera na mipango kuelekea kufikia lengo hilo.
Aidha amebainisha kuwa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi uso kwa uso kutasaidia kuwalinda watu walio katika mazingira magumu zaidi wakati wa kujikwamu kutoka klwenye janga la Corona( COVID-19) na kipaumbele cha kwanza sasa hivi ni kuweka mipango na sera kuzuia mitambo mipya ya makaa yam awe na kuacha matumizi ya makaa ya mawe ifikapo mwaka 2040.
Ameongeza kuwa “nchi zilizoendelea bado hazijatimiza ahadi ya kila mwaka ya dola bilioni 100 kwa juhudi za hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kusaidia jamii zilizo katika mazingira magumu ambazo tayari zinateseka na athari za ongezeko la joto duniani.”
Amefafanua kuwa mtu mmoja kati ya watatu ulimwenguni bado hawajafanikiwa vya kutosha na mifumo ya tahadhari ya mapema, ambapo wanawake na wasichana, ambao ndio asilimia 80 ya wale wanaolazimika kuhama kutokana na dharura ya mabadiliko ya tabianchi, bado mara nyingi hutengwa na maamuzi ya kushughulikia changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
mwisho
Discussion about this post