MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (EWURA), imetoa msaada wa mashuka 431 yenye thamani ya Sh.Milioni tano kwa vituo vinne vya afya vilivyopo jijini Dodoma ili kusaidia uboreshaji wa huduma za afya’
hilo ambalo linakabiliwa na ongezeko la idadi ya watu.
Akizungumza mara bada ya kukabidhi msaada huo Kaimu Mkurugenzi wa EWURA, Mhandisi Godfrey Chibulunje,amesema kuwa wametoa msaada huo ili kuongeza kasi ya utoaji huduma za afya kwa wananchi kupitia vituo vya afya vinne ambavyo ni Makole, Mkonze, Hombolo na Kikombo.
Mhandisi Chibulunje amesema Jiji la Dodoma ni kati ya majiji yayaokuwa kwa kasi na kuongeza idadi ya watu hivyo msaada huo wameutoa ikiwa ni mchango wa mamlaka hiyo kwa jamii hususan katika kipindi hiki cha kuhitimisha wiki ya utumishi wa umma nchini .
Amesema kuwa msaada huo utasambazwa katika vituo vya afya vilivyolengwa kwa kuzingatia mahitaji halisi katika kila kituo.
“Tumetoa msaada wa mashuka 431 kwa Jiji la Dodoma na yataenda kwa vituo vinne cha Makole, Hombolo, Mkonze na Kikombo na sisi mwaka huu tumechagua eneo la afya ili kusaidia jamii”amesema Mhandisi Chibulunje.
Mhandisi Chibulunje ameongeza kuwa katika kuadhimisha wiki ya utumishi wa umma, mamlaka hiyo imetoa mafunzo kwa watumishi wake na kutembelea watoa huduma mbalimbali wanaowasimamia kubaini changamoto wanazokabiliana nazo ili waweze kuzitatua kwa kuwa lengo lao ni kuhakikisha mlaji anapata huduma bora kwa viwango vinavyosimamiwa na mamlaka yao.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dk. Andrew Method,amesema msaada huo utatumika kama ulivyopangwa na kwamba wanaishukuru EWURA kwa msaada huo
Amesema wanaishukuru EWURA kwa kuendelea kusaidia sekta ya afya katika jiji hilo ambapo tayari ilikwishatoa msaada wa vifaa vya kutunza watoto njiti
Dk.Method amesema kwa mwezi katika Kituo cha Afya cha Makole wajawazito wanaojifungua ni zaidi ya 400 ambapo kwa wastani , wajawazito 120 wanajifungua kila wiki.
mwisho
Discussion about this post