CANADA imekumbwa na joto kali linalofikia nyuzi joto 46.1 hali iliyosababisha migahawa, maduka na shule kufungwa katika baadhi ya maeneo.
Mbali na kufungwa kwa shule na shughuli zingine za kijamii theluji pia imeyeyuka na kusababisha kuongezeka kwa kina cha maji ya mto, hali iliyopeleka wananchi kuhamishwa.
Wimbi hilo la joto, limeathiri zaidi magharibi mwa nchi hiyo, limesababisha msimu wa joto mkali zaidi katika miaka 84 iliyopita nchini humo.
Kulingana na Huduma ya Hali ya Hewa ya Canada, joto la nyuzi 46.1 lililorekodiwa katika jimbo la British Columbia juzi alasiri na kurekodiwa kama joto la juu kabisa kuwahi kutokea nchini humo.
Rekodi ya awali ya joto la juu katika historia ya nchi hiyo ilikuwa nyuzi 45 Celsius, iliyorekodiwa katika jimbo la Saskatchewan mnamo Julai 1937.
Wakati joto hilo likiongezeka,imeripotiwa kuwa theluji iliyeyuka haraka zaidi ya inavyotarajiwa kwa sababu ya joto hilo, ambapo nyumba nyingi zimehamishwa kutokana na kuongezeka kwa viwango vya maji katika mto.
Mtaalam wa hali ya hewa katika Wizara ya Mazingira ya hiyo Derek Lee, ,amekielezea chombo cha habari cha CBC kuwa joto litapanda zaidi kutoka nyuzi 46.1 hadi kuweza kufikia nyuzi joto 50 za Celsius katika maeneo mengine.
Kwa upande mwingine, vituo vya kupoza joto vimefunguliwa katika baadhi ya maeneo mengi kati miji ya nchi hiyo dhidi ya athari mbaya za hali ya hewa ya joto.
Haya hivyo kliniki ambazo zinatoa chanjo ya ugonjwa wa corona(COVID-19) zimeamua kuahirisha kazi zake.
Kuongezeka kwa viwango vya joto duniani kunasababishwa na mabadiliko ya tabia nchi hasa uchafuzi wa hali ya hewa.
Moja ya athari mbaya zaidi za ongezeko la joto ni kuibuka kwa moto katika maeneo mbali mbali ya misitu duniani hali inayopelekea maelfu ya watu kuhamishwa ambapo moja kati ya nchi inayoathirika sana na ongezeko la joto ni Australia.
Athari za mabadiliko ya tabia nchi zimeendelea kuiathiri dunia kwa kuongezeka viwango vya joto kali huku baadhi ya miji ikitabiriwa kuzama kutokana na ongezeko la kina cha maji baada ya theluji kuyeyuka.
Shirika la Hali ya Hewa duniani (WMO) umeulelezea mwaka 2019 kama mwaka uliokuwa na joto kali zaidi duniani baaya ya mwaka 2016
MWISHO
Discussion about this post