• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

TAWA:Chatu ndiye nyoka mkubwa pekee asiye na sumu

by BAJETI
July 1, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori  Tanzania (TAWA) imesema Chatu ndiyo nyoka pekee asiye na sumu mwenye uwezo wa kuishi miaka 20 hadi 25.

Hayo yameelezwa leo mkoani Dar es Salaam na Ofisa Utalii wa TAWA Gregory Kalokole wakati akizungumza na wananchi  waliotembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ‘ Uchumu wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu’ kujionea wanyama mbalimbali wakiwemo Simba,Chui,Fisi,Mamba na aina ya ndege wakubwa wakiwemo Tai.

Amesema kuna wa nyoka wa aina nyingi lakini Chatu hukua na kufikia urefu wa mita tatu hadi nne na uzito wa kilo 44 hadi 55 ambapo hupendelea kuishi katika ,maeneo yenye vichaka,nyasi ndefu na fupi,miamba na  misitu.

Amefafanua kuwa chatu huwa na tabia ya kujiviringisha hata akiwa juu ya mti lakini wa  kike hujiviringisha katika maeneo aliyotaga mayai ili kuyalinda na huchukua siku 90 kujiangua na watoto kutoka.

“Kuna nyoka wengi sana lakini Chatu ndiye aina ya nyoka pekee asiye na sumu na mawindo yake ni katika maeneo yenye vichaka na hupendelea kula Panya ,Swala,Tumbili,Mbwa na wengine wa jamii hizo na baada ya kuwakamata hubana na kuvunja na kisha kutoa mate yenye utelezi ili aweze kumeza kwa urahisi.”amesema Kalokole

Kalokole ameongeza kuwa Chatu hupendelea wanyama wenye damu joto na baada ya kumeza chakula chake hukaa eneo hilo hadi kitakapooza tumboni ambapo hutegemea na aina ya mnyama aliyemmeza na  ikiwa ana pembe kichwa hukiacha nje.

“Adui mkubwa wa Chatu ni ndege wakubwa kama Tai na binadamu na kwamba anapatikana katika maeneo yote ya Tanzania hata kwenye makazi ya binadamu ikiwa tu kuna vyakula vyake na mazingira ya vichaka na misitu”amesema Kalokole.

Kalokole amefafanua kuwa  TAWA inasimamia wanyamapori wote walioko nje ya Hifadhi za Taifa  na Ngorongoro na katika maeneosho hayo ya Sabasaba wamepeleka pia wanyama wengine wakiwemo Simba na Chui hivyo ni fursa kwa watanzania kutembelea eneo hilo kujifunza.

“Wanyama wengine kama Chui huwa na tabia tofauti ambapo wengine hupendelea kukaa peke yao  na ndio maana huyu tuliyemleta hapa ni aina hiyo wanaopenda kuishi peke yao”amesema Kalokole

Next Post

Pikipiki zapigwa marufuku Afghanistan

Mfuko wa Misitu wawezesha miradi zaidi ya 500 kuboresha maisha ya wananchi

TGDC: Megawati 5000 nishati ya jotoardhi hazijaendelezwa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In