• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mfuko wa Misitu wawezesha miradi zaidi ya 500 kuboresha maisha ya wananchi

by BAJETI
July 2, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

MFUKO wa Misitu Tanzania umewezesha miradi zaidi ya 500 nchini ili kuboresha uhifadhi na usimamizi  wa rasilimali misitu, ardhi na mifumo ya ikolojia kwa kutoa ruzuku.

Ruzuku hizo ambazo hutolewa kwa wadau wote wanaojihushisha na usimamizi wa rasilimali za misitu na uboreshaji wa hali ya maisha ya wananchi waishio pembezoni mwa misitu.

Hayo yameelezwa leo mkoani Dar es Salaam katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ‘ Uchumu wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu’.

Mfuko huo ulio chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii ni Mfuko wa hifadhi ambao umeanzishwa kisheria kama njia endelevu ya kuwezesha uhifadhi wa rasilimali za misitu hapa nchini na kukabiliana na changamoto za usimamizi wa rasilimali za misitu hasa katika utekelezaji wa Sera na Sheria ya Misitu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Mfuko huo hutoa ruzuku za aina tatu ambazo zinatofautishwa na kiasi cha fedha kitolewacho,walengwa  na muda wa utekelezaji wa miradi.

Ruzuku hizo ni pamoja na ruzuku ndogo za kiasi cha fedha kisichozidi Sh.Milioni tano kinachotolewa kwa watu binafsi na vikundi ili kugharamia utekelezaji wa miradi midogo.

“Ruzuku ya kati ambayo ni kiasi kinachozidi Sh.Milioni tano na kisichozidi Sh.Milioni 20 na ruzuku kubwa ni kiasi kinachozidi Sh.Milioni 20 na kisichozidi Sh.Milioni 50 na hutolewa ili kugharamia miradi inayochukua muda mrefu”imeeleza taarifa hiyo.

Aidha imefafanua kuwa baadhi ya majukumu ya mfuko ni kutoa ruzuku kwa wadau wa misitu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya uhifadhi na uendelezaji wa misitu katika maeneo ya usimamizi yaliyopo nje ya maeneo ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Hata hivyo taarifa hiyo imebainisha matatizo yanayoukabili Mfuko huo kuwa ni pamoja na kukabiliwa na uhaba wa fedha kulingana na matarajio ya wadau  ambapo kwa sasa chanzo cha mapato ya Mfuko ni serikali kutoka kwenye vyanzo vilivyoainishwa kwenye Sheria ya Misitu ya Mwaka 2002.  

Taarifa hiyo imewataja wadau wa Mfuko huo ni pamoja na Jamii,Asasi za Kijamii,watafiti na Taasisi za Utafiti,wanamazingira,Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Wadau wengine ni pamoja na Taasisi za mafunzo ya misitu na nyuki,Wizara ya Maliasili na Utalii,Serikali za Mitaa zikiwemo Halmashauri za Wilaya,Taasisi zisizo za kiserikali (NGOs) na Asasi za kiraia.

Next Post

TGDC: Megawati 5000 nishati ya jotoardhi hazijaendelezwa

Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere kujazwa maji ifikapo Novemba

TGDC kuanza kuchoronga visima nishati jotoardhi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In