KAMPUNI ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania (TGDC) imesema inatarajia kuchoronga visima vitatu vya utafiti na uhakiki wa nishati ya jotoardhi(majimoto) nchini.
TGDC ambayo ni Kampuni Tanzu ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) chini ya Wizara ya Nishati ilianzishwa Desemba 2013 ili kukabiliana na upungufu wa uzalishaji wa umeme wa kutosha kutokana na sababu mbalimbali ambapo serikali iliamua kuwa na vyanzo vingine vya uzalishaji wa umeme vya nishati jadidifu ikiwemo jua,upepo na jotoardhi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na TGDC mkoani Dar es Salaam katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ‘ Uchumu wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu’ imesema kuwa maeneo saba waliyafanyia utafiti na uhakiki wa kisayansi lakini matatu kati ya hayo ndiyo watachoronga visima.
Taarifa hiyo ya TGDC imefafanua kuwa mpaka sasa kuna maeneo zaidi ya 52 yenye viashiria vya nishati ya jotoardhi (maji ya moto) yanayotoka chini ya ardhi kutokana na tafiti za awali za kisayansi.
Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa hadi kufikia mwaka 2018 TGDC ilikuwa imefanya tafiti zaidi kwenye maeneo ya Songwe-Songwe,Ngozi-Mbeya,Mbaka Kiejo-Mbeya,Luhoi-Pwani,Ibadakuli-Shinyanga,Kisaki-Morogoro na Natron-Arusha
“Lakini hadi kufikia Januari 2019 maeno yaliyokuwa yamefakwisha fanyiwa tafiti na yalikuwa kwa uchorongaji wa visima vya utafiti na uhakiki wa nishati ya jotordhi ni Ngozi mkoani Mbeya,Mbaka Kiejo mkoani Mbeya pia na Songwe mkoani Songwe”imeeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa baada ya uchorongaji visima vya utafiti na uhakiki ,hatua itakayofuata ni uchongaji visima vya uzalishaji.
Taarifa hiyo ilifafanua pia kuhusu Ziwa Ngozi lililopo mkoani Mbeya ambapo linauhusiano wa moja kwa moja na nishati ya jotoardhi kutokana na kwamba lina viashiria vya chemichemi za majimoto chini ya Ziwa hilo pamoja na kemikali zinazopatika katika maji yake.
“Asili ya Ziwa Ngozi inatokana na mlipuko wa volkano ambayo kisayansi ina uhusiano wa moja kwa na nishati ya jotoardhi ambapo vielelezo vya kisayansi vinafafanua kuwa nishati ya joto ardhi inatokana na joto asilia linalozalishwa katikakati ya tabaka au kitovu cha duani”imeeleza taarifa hiyo.
Discussion about this post