AFGHANISTAN imepiga marufuku matumizi ya wa pikipiki ikiwemo kusafiria katika Mji Mkuu wa nchi hiyo Kabul.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo Tarık Aryen amesema uendeshaji wa pikipiki ni marufuku katika maeneo ya Kabul na wilaya zingine za nchi hiyo.
Amesema wanatarajia wananchi wataunga mkono hatua hiyo na vikosi vya usalama na wale ambao watakiuka hatua hiyo pikipiki zao zitachukuliwa
Hata hivyo sababu za kiusalama ndio zilizosababisha hatua hiyo baada ya kundi la Taleban kuongeza mashambulizi zaidi dhidi ya maeneo yanayomilikiwa na serikali ya nchi hiyo
Wakati mchakato wa amani nchini Afghanistan bado hauna uhakika, mashambulizi yameonekana kuendelea.
Idadi ya wilaya zilizo chini ya udhibiti wa Taliban katika miezi miwili iliyopita imezidi 45.
Kulingana na data ya Umoja wa Mataifa, Taliban inadhibiti asilimia 50 hadi 70 ya eneo la nchi hiyo, isipokuwa vituo vya mijini
Discussion about this post