• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

TANESCO yaeleza faida za mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere(JNHPP)

by BAJETI
July 5, 2021
in Habari
0
Share on FacebookShare on Twitter

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) limesema kukamilika kwa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere kwa kutumia maji ya Mto Rufiji(JNHPP ) utalefa faida nyingi ikiwemo nchi kuwa na umeme wa zaida na kuondoa mafuriko.

Mradi huo unaotarajiwa kukamilika Juni  14,2022 utazalisha megawati 2115 za umeme ambapo hadi kufikia mwezi mei 2021 ulikuwa umefikia asilimia 52 ya ujenzi wake.

Akizungumza leo mkoani Dar es Salaam katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ‘ Uchumu wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu’Mhandishi wa TANESCO Mwanji Mhaka amesema ujenzi wa bwawa hilo una  faida nyingi ikiwemo  kuondoa tatizo la mafuriko katika baadhi ya vijiji vilivyokuwa vikikumbwa na tatizo hilo.

Amesema hadi kufikia Juni 2022 bwawa hilo  litakuwa na mita za ujazo Bilioni 32.3 ili kuanza kuzalisha umeme hivyo maji ya Mto Rufiji yatakuwa katika mtiririko maalum ambao utasaidia kuondoa tatizo la mafuriko katika baadhi ya maeneo kama Ikwiriri,Mtanza na Mloka.

Amesema mbali na kuondoa mafuriko lakini pia  kutakuwa na kilimo cha umwagiliaji katika ukubwa wa heka 200,000 ambapo wakulima watafaidika na mradi huo.

“Kutakuwa na uvuvi na ufugaji na wanyama wengi watapata maji na hawatasafiri umbali mrefu sana ,kushuka kwa bei za umeme na kuwa na umeme wa uhakika pamoja na utalii ambapo  wanyama wengi watazunguka bwawa.

“Itavutia wawekezaji kwa kuwa na umeme wa uhakika na ndani ya bwawa kutakuwa na visiwa ambapo pia kunaweza kujengwa hoteli za kitalii kutokana na kwamba bwawa hilo litakuwa na ukubwa wa kilomita za mraba 55,000.”amesema Mhaka

Mhandisi Mhaka ameongeza kuwa kushuka kwa bei ya umeme kutachochea zaidi wananchi kutumia nishati hiyo na kuachana na matumizi ya kuni hivyo kulinda mazingira.

“Mahitaji ya umeme nchi nzima ni megawati 1,300 na uzalishaji katika vyanzo vyote ni megawati 1601 na Julius Nyerere litazalisha megawati 2115 kwa maana hiyo tutakuwa na umeme mwingi wa ziada hali itakayoongeza ukuaji wa uchumi”amesema Mhaka

Hata hivyo Mhaka amebainisha kuwa kuna miradi mingine ya kijamii itajengwa katika vijiji vilivyopo karibu na bwawa hilo mara tu uzalishaji wa umeme utakapokuwa unaendelea.

Next Post

TMDA:Kunusa na kuweka ugoro mdomoni ni kosa kisheria.

Mradi wa Julius Nyerere umezalisha ajira zaidi ya 7400

TANESCO:Mradi wa JNHPP unalinda mazingira.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In