• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mzumbe yawezesha vijana kujiajiri

by BAJETI
July 6, 2021
in Habari
0
Share on FacebookShare on Twitter

CHUO Kikuu cha Mzumbe wameweka mifumo ya kutoa mafunzo mbalimbali ili kuwasaidia vijana kuweza kujiari pindi wanapomaliza masomo yao

Chuo hicho kina kituo cha Uwatamizi na Malezi ya vijana  ili  kujifunza vitu mbalimbali ambapo zaidi ya vijana 20 wameshajiari.

Hilo limejitokeza juzi,katika banda la chuo hicho katika Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba yenye kauli mbiu ‘ Uchumu wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu’.

Mmoja wa wanafunzi wa chuo hicho wa Shahada ya Sayansi ya Uzamili katika Mipango na Menejimenti ya  Miradi Kampas ya Morogoro Nelson Kisanga amesema

wapo katika kituo cha Uwatamizi na Malezi ya vijana  chuoni hapo kujifunza vitu mbalimbali.

Amesema kupitia kituo hicho wametengeneza mfumo wa Aquaponics ambao unajumuisha ufugaji wa samaki na kilimo cha mboga mboga.

Kisanga amesema wametengeneza mfumo huo ambao chini wanafuga samaki na juu wanafanya kilimo cha mbogamboga lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya ajira.

Kisanga ameongeza kuwa  mbali na mfumo huo lakini pia wanabadilisha taka na kuwa  wadudu kwa ajili ya chakula cha mifugo kama vile kuku, Nguruwe na hata samaki.

“Tunafanya vitu vingi pia kituo hiki kimetusaidia vijana kufika mbali kwani tayari tumeshasajili kampuni yetu ya Real Agriculture Group,” amesema Kisanga.

Ameongeza kuwa kupitia kituo hicho wameweza kuongeza mnyororo wa thamani kwa kukuchakata viazi lishe na kupata unga kwa ajili ya kutengeneza juisi, chapati na mikate.

Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo hicho Kampas ya Morogoro  Dkt. Bahati Ilembo, amesema Chuo Kikuu cha Mzumbe kinatoa program nyingi za ujasiriamali  na kwamba  kituo cha Uwatamizi kinahusika kukuza vipaji vya vijana.

” Tunakuza vipaji vyao kwa kukusanya mawazo yao na ubunifu wanapokuwa katika kituo hiki wanajengwa na kuongezwa uwezo ili mawazo yao ya ubunifu yaweze kuwasaidia,” amesema.

Mhadhiri huyo ameeleza kuwa wana vijana takribani 50 ambao wameweza kuendelezwa kati yao 20 tayari wanajitegemea kwa kutengeneza bidhaa zao na kuuza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chuo hicho Rose Joseph ameeleza kuwa wana mfumo uliowekwa kwenye masomo ya kibiashara, teknolojia na ubunifu ambao unaendana na kauli mbiu ya mwaka huu katika Maonyesho hayo.

” Kwa misingi ya kuunga mkono serikali katika kuinua uchumi na kufikia wa kati. Tuna changamoto kubwa ya ajira vijana wanamaliza vyuo vikuu wanabaki kuzurura mitaani na karatasi kutafuta kazi “amesema Joseph

Joseph amefafanua kuwa Chuo cha Mzumbe kimelenga kumsaidia kijana kuondokana dhana ya kuajiriwa baada ya kumaliza masomo yake kwa kumjengea uwezo wa kubuni vitu ili wanapomaliza wawe na miradi mikubwa na kuweza kuajiri vijana wengine.

Next Post

Baba Mtakatifu ateuwa maaskofu Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Kwaya KKKT kuanzisha kiwanda cha kusindika nyama

Tani bilioni 8.5 za barafu zayeyuka baada ya joto kuongezeka Greenland.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In