BABA Mtakatifu Fransisko amewateua mapadre wawili kuwa Maaskofu Wasaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 7,mwaka huu kwa vyombo vya habari mkoani Dar es Salaam na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na kusainiwa na Katibu wa Baraza hizo Padre Charles Kitima mapadre hao walioteuliwa kuwa Maaskofu ni wa Shirika la Waagustiniani(O.S.A)
Padre Kitima amewataja maaskofu wateule hao kuwa ni Mhashamu Askofu Henry Mchamungu na Askofu Stephano Lameck Musomba ambao watakuwa Maaskofu Wasaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.
“Mhashamu askofu mteule Henry Mchamungu alizaliwa Januari 18 mwaka 1965 huko Legho Kilema jimboni Moshi”amefafanua Padri Kitima
Amesema baada ya masomo yake ya upadre alipewa daraja takatifu la upadre Juni 24,1994 na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume Jimbo Kuu la Dar es Salaam na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
“Hadi uteuzi wake ,askofu mteule alikuwa Mwalimu na mlezi Seminari ya Segerea ,Dar es Salaa.”amesema Padre Kitima
Padre Kitima aliongeza kuwa Mhashamu askofu mteule Stephano Lameck Musomba alizaliwa Septemba 25, 1969 huko Malonji jimboni Mbeya.
“Baada ya masomo yake ya upadre,alipewa daraja takatifu la upadre Julai 24,2003 na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume wa Shirikani na jimboni Dar es Salaam na Morogoro.
“Hadi uteuzi wake,askofu mteule alikuwa Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili-Mavurunza ,Dar es Salaam na Katibu wa Shirika lake la Waangustiniani Kanda ya Tanzania”amesema Padri Kitima
Discussion about this post