NA MWANDISHI WETU ARUSHA
DC Mjema awafunda TRA
MKUU wa Wilaya ya Arusha Sophia Mjema ameitaka Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kukutana na wafanyabiashara ili waweze kujadili na kujenga mahusiano bora katika utendaji wao wa kazi.
Mjema ametoa wito huo leo jijini Arusha mara baada ya kuzindua kampeni ya kuhamasisha matumizi ya mashine za kutolea risiri za kielektroniki (EFD) Kanda ya Kaskazini.
Mjema amesema ametoa wito huo kufuatia agizo lililotolewa na Rais Samia Suluhu Hasan la kuitaka TRA kujenga mahusiano mazuri kati yao na wafanyabiashara.
Amefafanua kuwa TRA imekuwa na mchango mkubwa katika ukusanyaji wa kodi na tozo mbalimbali ambazo zimekuwa zikisaidia kwa kiasi kikubwa serikali ya awamu ya sita kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi anaehusika na ukusanyaji wa kodi mkoani Arusha Malaki Nyage amesema kampeni hiyo inalenga kutoa elimu kwa wafanyabiashara pamoja na kutambua umuhimu wa kutumia mashine za kutolea risiti ya EFD.
Naye mfanyabishara Adeline massawe amebainisha namna mashine za EFD zinavyofakazi ikiwemo kuwasaidia wafanyabiashara kutunza kumbukumbu zao za malipo.
Discussion about this post