Warning: Attempt to read property "child" on null in /home/bajetico/public_html/wp-content/themes/hilonga/class/ContentTag.php on line 45
  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mabadiliko ya tabianchi yaathiri Sekta ya Kilimo Bara,Zanzibar wizi wa mazao wakithiri.

by BAJETI
August 19, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

MABADILIKO ya tabianchi yametajwa kuwa ni kikwazo kikubwa katika Sekta ya Kilimo Tanzania Bara huku Tanzania Zanzibar ikikabiliwa na wizi wa mazao.

Hayo ni kwa mujibu wa  Sensa ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Mwaka wa Kilimo 2019/20 katika Ripoti ya Matokeo Muhimu kwa Sekta za mazao,mifugo na ufugaji wa samaki iliyotolewa Agosti mwaka huu na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)

Sensa hiyo imeonesha kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaonekana kuwa ni changamoto kubwa inayoikabili sekta ya kilimo kwa Tanzania Bara ikifuatiwa na gharama za pembejeo ikilinganishwa na Zanzibar ambayo inakabiliwa na changamoto kubwa za wizi wa mazao na uhaba wa ardhi.

“Matokeo ya Sensa yanaonesha kuwa, kaya nyingi zilikutana na vikwazo mbalimbali katika Mwaka wa Kilimo 2019/20.

“Baadhi ya vikwazo vikubwa muhimu vilivyoripotiwa na kaya katika shughuli za kilimo ni mabadiliko ya tabianchi (ukame, mafuriko; asilimia 17.8), gharama za pembejeo (asilimia 15.6), upatikanaji wa ardhi (asilimia 13.5), bei ndogo za mazao (asilimia 7.2), magonjwa na wadudu waharibifu (asilimia 6.7), upatikanaji wa pembejeo (asilimia 5.6) na rutuba ya udongo (asilimia 5.6).imeeleza taarifa hiyo.

Katika ujumbe muhimu wa Sensa hiyo umeongeza kuwa mabadiliko ya tabianchi yataendelea kuathiri sekta za mazao na mifugo na hivyo kupungua kwa tija katika uzalishaji.

Hata hivyo imependezwa kuwa kuendeleza kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, kilimo cha umwagiliaji na utafiti na matumizi wa mbegu zinazohimili mabadiliko ya tabianchi ni muhimu.

Aidha katika ujumbe muhimu wa taarifa hiyo imebainisha kuwa kutokana na uhaba wa ardhi uliopo Zanzibar, ni muhimu kutoa kipaumbele kutumia eneo dogo kwa kuongeza uzalishaji.

“Kwa upande wa Tanzania Zanzibar, matokeo ya Sensa yanaonesha kuwa, wizi wa mazao (asilimia 20.8) ni kikwazo kikubwa kilichoathiri shughuli za kilimo kwa mwaka wa kilimo 2019/20, ikifuatiwa na upatikanaji wa ardhi (asilimia 12.0), uharibifu wa wanyama/ndege (asilimia 11.0),

“Magonjwa na wadudu waharibifu (asilimia 11.0), gharama za pembejeo (asilimia 6.8), upatikanaji wa pembejeo (asilimia 5.1) na wizi wa mifugo (asilimia 5.1)”imefafanua taarifa hiyo

Next Post

Makalla ataka waliojiunganishia mabomba ya mafuta wajisalimishe

Rais mstaafu ataka kujinyonga

Aliyepata chanjo ya COVID-19 kutambuliwa kimataifa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In