KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mwanaharakati wa kikundi cha kupambana na rushwa maarufu kama (Lucha) nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) Ghislain Muhiwa amekamatwa wakati akipeleka mahari kwa wakwe zake.
Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa Muhiwa amekamatwa baada ya kumtuhumu mke wa Rais wa nchi Felix Tshisekedi kwa ubadhirifu wa mali ya umma.
Mtuhumiwa huyo alikamatwa akiwa anaelekea Goma nchini humo kutoa mahari kwa wakwe zake.
Kundi la vijana la kupigania mageuzi, maarufu kamaLucha , linatuhumu kwamba taasisi inayosimamiwa na mke wa Rais, Denise Tshisekedi, imepora msaada uliyokuwa umelengwa kuwapa waathiriwa wa mlipuko wa volcano katika mlima Nyiragongo, mashariki wa nchi DRC.
Hata hivyo taasisi ya mke wa Rais huyo imekanusha tuhuma hizo za ubadhirifu wa mali ya umma.
Muhiwa anakuwa mwanachama wa pili wa kundi hilo kukamatwa baada ya mwenzake Parfait Muhani aliyekamatwa mwezi Julai mwaka huu kwa madai hayo hayo ambapo anasubiri kesi yake mbele ya mahakama ya kijeshi.
Discussion about this post