• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Fukwe za Dar es Salaam kuwa za kitalii

by BAJETI
August 24, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amesema Fukwe zote za Mkoa huo yakiwemo maeneo ya wazi zitaboreshwa na kuwa sehemu ya utalii.

Makalla amesema amefanikiwa kupata wadau waliokubali kuwajengea wafanyabiashara wa ufukwe wa Coco vibanda vya kisasa na kuboresha mandhari ya ufukwe huo ili uwe kwenye mwonekano wa Kisasa.

Makalla ametoa kauli hiyo leo Agosti 24,2021 mkoani Dar es Salaam mara baada ya kutembelea ufukwe huo akiambatana na Viongozi kutoka Wilaya ya Kinondoni na wadau waliokubali kuwa sehemu ya maboresho ya fukwe  hizo.

Akizungumza na wafanyabiashara wa eneo hilo Makalla amesema dhamira yake na serikali ni kuona Fukwe zote za Mkoa wa Dar es Salaam zinaboreshwa ikiwemo Coco kuwa ya kisasa na shughuli za utalii.

Makalla ameongeza kuwa ni muhimu kwa Manispaa ya Kinondoni kuanza ujenzi wa Ofisi na vyoo vya kisasa ikiwemo kupeleka umeme katika eneo lote la ufukwe huo.

Mpango wa kuboresha Fukwe za Dar es salaam unaenda sambamba na maboresho ya maeneo ya wazi, bustani za kupumzika, usafi na upandaji wa miti, maua na kingo pembezoni mwa Barabara.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla (wa kwanza mbele)akisoma maelezo kuhusu utumikaji wa mfumo mpya wa ukusanyaji ushuru wa maegesho jijini Dar es Salaam leo(Picha na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam)

Wakati huo huo Makalla amezindua mfumo wa kukusanya ushuru wa maegesho kidigitali ambapo fedha zote zitapokelewa moja kwa moja serikalini.

 Amesema mfumo huo utaondoa rushwa na  uonevu  ambapo utaongeza ufanisi katika ongezeko la mapato.

Makalla amefafanua kuwa mfumo huo utaanza rasmi kutumika Septemba mosi mwaka huu na utaenda kutatua kero na changamoto mbalimbali zilizokuwa zinajitokeza

Next Post

Asilimia 50 ya kuku wapata chanjo

Makalla kumaliza kero ya ardhi Dar es Salaam

Daraja la Selander lakamilika asilimia 91

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In