• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Daraja la Selander lakamilika asilimia 91

by BAJETI
August 26, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

DARAJA jipya la Selander linalopita baharini mkoani Dar es Salaam limekamilika kwa asilimia 91 ambapo kazi iliyobaki ni kuunganisha eneo la juu pekee ili lianze kutumika.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) ambayo imeelezea hatua zilizofikiwa hadi sasa juu ya ujenzi wa daraja hilo.

“Daraja jipya la Selander limekamilika kwa asilimia 91,na wakati ujenzi wa daraja hili ukimaliziwa,kazi inayoendelea sasa ni kuunganisha eneo  la juu la Daraja,miundombinu bora ya barabara ,madaraja na viwanja vya ndege ni kwa maendeleo ya Taifa”alieleza taarifa hiyo.

Muonekano wa Daraja la Selander mkoani Dar es Salaam ulivyo sasa(Picha na mpigapicha wetu)

Darala hilo linajengwa kwa gharama ya Sh.Bilioni 243 ambalo ni  la kipekee Afrika Mashariki na Kati  na lilizinduliwa ujenzi wake Julai 23, 2018 na Hayati Rais Dkt.John Magufuli.

Daraja hilo ambalo ujenzi wake ukiwa ni wa miezi 36 sawa na miaka mitatu, huku likiwa na urefu wa Kilomita 6.23 ambapo kati ya hizo Kilomita 1.03 ni daraja na Kilomita 5.2 ni barabara unganishi.

Hadi kukamilika kwake litaunganisha barabara ya Barack Obama na eneo la Fukwe za Coco(Coco Beach)katika makutano ya barabara za Kenyatta na Toure.

TANROADS imekuwa Wakala bora wa Serikali kutokana na kujijengea heshima ya kusimamia kikamilifu miundombinu ya barabara na madaraja makubwa nchini hali inayoongeza thamani ya pesa za walipa kodi na kutatua kero za wananchi.

Daraja la Selander(Salenda) jijini Dar es Salaam likiwa katika hatua za kukamilika kwake ili lianze kutumika(Picha na mpigapicha wetu)

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikiendeleza miradi yote iliyoanzishwa na Serikali ya Awamu ya Tano ya Hayati Rais John Magufuli kwa kuhakikisha kuwa fedha zinapatikana ili kukamilisha miradi hiyo.

Next Post
Korosho yaongoza uzalishaji mazao ya biashara

Korosho yaongoza uzalishaji mazao ya biashara

Maziwa ya mbuzi yafikia lita milioni 25.7

Makalla amuonya mkandarasi barabara ya Makongo

Makalla amuonya mkandarasi barabara ya Makongo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In