• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Makalla amuonya mkandarasi barabara ya Makongo

by BAJETI
November 22, 2021
in Habari
0
Makalla amuonya mkandarasi barabara ya Makongo
Share on FacebookShare on Twitter

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amesema haridhishwi na kasi ndogo inayofanywa na Kampuni ya JASCO inayojenga barabara ya Makongo na kumtaka kuikabidhi barabara hiyo ifikapo Oktoba 8,2021.

Amesema Serikali imefanya kila kitu ikiwemo kulipa fidia,kuondoa miundombinu mingine ili ujenzi wa barabara hiyo ufanyike kwa haraka na bila visingizio lakini kasi ya Kampuni hiyo katika ujenzi hairidhishi.

Makalla ameyasema hayo jijini Dar es Salaam mara baada ya kutembelea eneo la Makongo ambako mradi huo wa ujenzi wa barabara unafanyika.

“Habari ya Makongo mimi sitaki tena kusikia,mimi ni mwenyeji,mimi nilikuwa Mwenyekiti wa Kata hii,naomba mradi huu wa Makongo ukamilike kwa wakati visingizio vyote hatutaki”amesema Makalla

Hata hivyo Makalla ameonyesha kuchukizwa na tabia ya mkandarasi huyo kuonekana eneo la kazi siku pekee ambayo viongozi wanatembelea barabara hiyo jambo linalosababisha kusuasua kwa mradi huo na kuleta kero na mateso kwa wananchi.

“Tayari  Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA),Shirika la Umeme nchini(TANESCO) na Kampuni ya Simu nchini(TTCL) wameondoa miundombinu yao na wananchi wote wamelipwa fidia walizokuwa wakidai hivyo sioni sababu yoyote ya mkandarasi huyu kuchelewesha mradi”amesema Makalla

 

 

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla (Kulia) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe jana jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi wa barabara ya Makongo inayojengwa kwa kiwango cha lami na Kampuni ya JASCO (Picha na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam)

 

 

Barabara hiyo ya Makongo ina urefu wa Kilomita 4.5 na ujenzi wake unagharimu zaidi ya Sh. Bilioni nane  ambapo ikikamilika itasaidia kurahisisha usafiri kwa wakazi wa Makongo na Goba ikiwemo kupunguza msongamano wa magari kwenye Barabara ya Bagamoyo.

Next Post

Wanahabari 124 wakimbilia Mexico

Kuku wa kisasa wafikia milioni 44.5

Kuku wa kisasa wafikia milioni 44.5

Chanjo ya Malaria,Kifua Kikuu kuanza kuzalishwa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In