MEXICO imetangaza kwamba imekubali kupokea wanahabari 124 na familia zao kutoka nchini Afghanistan ambao walihamishwa baada ya Kundi la Wanamgambo wa Taliban kuteka mji Mkuu wa nchi hiyo Kabul, Agosti 15,2021.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Mexico Marcelo Ebrard na wajumbe wake waliwakaribisha waandishi hao wa habari ambao walikuwa wakifanya kazi na mbalimbali yakiwemo ya kigeni pamoja na The New York Times, katika uwanja wa ndege uliopo Mji Mkuu wa nchi hiyo Mexico City.
Akizungumzia kuwasili kwa waandishi hao wa Kiafghanistan kupitia ukurasa wake wa kijamii,Ebrard amesema Mexico imeamua kuunga mkono maombi ya hifadhi ya kibinadamu.
“Maisha yote ya binadamu ni muhimu, lakini nataka kusisitiza kwamba kundi hili lililokuja Mexico leo linawakilisha uhuru wa vyombo vya habari na haki ya mawasiliano na maadili mengi yanayohusiana nayo.” Amesema Ebrard
Hata hivyo Mexico imesema waandishi hao waliomba ulinzi wa kibinadamu kutoka kwao

Rais Ashraf Ghani wa Afghanistan aliyekimbilia uhamishoni Dubai,Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E)
Maelfu ya raia nchini Afghanistan wamekuwa wakihamishiwa sehemu mbalimbali duniani wakikimbia utawala wa kundi la Taleban baada ya Serikali ya nchi hiyo kusambaratika.
Baadhi ya nchi zilizowapokean wakimbizi hao ni Uganda,Rwanda,Iran,Tajikistan,Uzbekistan,Pakistan,Ufaransa,Uingereza,Marekani,Canada,Urusi,Uhispania,Albania,Uturuki,India na zingine ambazo bado zinaendelea kuwapokea wakimbizi hao.
Agosti 31,2021 utakuwa muda wa mwisho wa majeshi ya Marekani na washirika wao kuondoka Afghanistan baada ya kuikalia nchi hiyo kwa miaka 20 kutokana na mashambulizi ya Septemba 11 mwaka 2001.

Discussion about this post