RAIS mpya wa Zambia Hakainde Hichilema ameteua wakuu wapya wa jeshi na kuwaondoa wakuu wote wa polisi huku akiahidi kumaliza utawala kandamizi wa mtangulizi wake Edger Lungu.
Hichilema aliyechukua madaraka wiki iliyopita amewahi kukamatwa mara nyingi katika maisha yake ya kisiasa na utawala uliopita.
Kupitia luninga ya Taifa Jumapili ya Agosti 29,2021), Hichilema alitangaza wakuu wapya wa Jeshi pamoja na wale wa Jeshi la Anga na kuwasimamishwa kazi mara moja makamishna wote bila kutoa maelezo zaidi na kuwataka polisi kufanya uchunguzi wa kina kabla ya kuwazuia washukiwa.

Alipoapishwa Jumanne wiki iliyopita, Hichilema aliahidi kumaliza ukandamizaji wa kisiasa pamoja na kufufua uhuru wa wanahabari, huku akiwahakikishia kwamba sasa hawatashambuliwa na gesi ya kutoa machozi au kufungiwa shughuli.
Discussion about this post