WAKATI baadhi ya nchi duniani zikijiwekea bajeti ya Sh.Trilioni 33 kwa mwaka mzima,Wizara ya Ulinzi ya Japan imezindua bajeti ya dola bilioni 50.
Uzinduzi huo umekuja wakati nchi hiyo ikiongeza matumizi ya kijeshi kufuatia vitisho vinavyozidi kuongezeka kutoka China na Korea Kaskazini.
Kwa mujibu wa DW,Bajeti ya jeshi imekuwa ikiongezeka nchini humo kwa takriban muongo mmoja huku Wizara ya Ulinzi ikionya kuwa mazingira ya kiusalama yanayoizunguka nchi hiyo yanazidi kuwa mabaya.
Wizara hiyo pia imesema inanuia kuongeza uwezo wake wa ulinzi wa anga na usalama wa kimtandao hata hivyo, fedha hizo ni kidogo ikilinganishwa na kiwango kilichoitishwa na Wizara hiyo mwaka uliopita.
Japan inapanga kuanza ujenzi wa meli tano za kijeshi na manowari, pamoja na kununua ndege za kivita aina ya F-35.
Discussion about this post