• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Sumu yaathiri mamia ya watu DRC

by BAJETI
September 1, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

MAMIA ya watu katika Jimbo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wamepatwa na ugonjwa wa kuhara ikiwemo kutokwa na vipele baada ya kutumia maji ya Mto Kasai yanayodaiwa kuwa na sumu.

Hata hivyo watu hao pia wanadaiwa kula samaki waliokufa kutokana na sumu hiyo iliyosambaa katika Mto Kasai ambao unapita katika jimbo hilo.

Maafisa wa serikali katika Jimbo la Kasai wamesema kuwa, maji ya mto mkoani humo yalibadilika rangi ambapo viboko na samaki waliokufa walikutwa kwenye maji hayo wakielea.

Sumu hiyo inadaiwa kutoka eneo la uchimbaji wa Almasi nchini Angola ambapo iliripotiwa kutoa kemikali za sumu tangu mwezi Julai mwaka huu ambazo zimechafua maji katika mito ya Kasai na Tshikapa nchini DRC. 

Naibu Waziri Mkuu anayeshugulikia Mazingira wa Eve Bazaiba amewaambia waandishi wa habari baada ya kulitembelea eneo lililoathirika kwamba zaidi ya kesi 4000 za kuhara zimesajiliwa katika maeneo 13 kati ya 18 yaliyoathiriwa katika jimbo la Kasai. 

Bazaiba ameongeza kuwa, wakazi wa maeneo yaliyoathirika wajiepushe na kula samaki waliokufa na matumizi ya maji ya mito hiyo 

Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Kasai wameeleza kuwa, wamepatwa na vijiupele mwilini baada ya kutumia maji hayo machafu.

Tayari serikali ya Kinshasa imechukua hatua za kuhakikisha kuwa, maji safi yanapelekwa katika maeneo yaliyoathirika.

Hofu imetanda katika Mto Kongo ambao ni wa pili kwa urefu barani Afrika ukitanguliwa na Mto Nile kwamba nao pia unaweza kukumbwa na hali hiyo kutokana na Mto Kasai kuingiliana na mto huo.

Next Post

Mwenyekiti Halmashauri Meru ataka wananchi kuchangia maendeleo

Wagonjwa afya ya akili waongezeka

Kiini migogoro ya ardhi Dar es Salaam chafichuliwa.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In