MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amesema migogoro mingi ya uvamizi wa ardhi inatokana na Taasisi zinazomiliki maeneo hayo kuyatekeleza kwa muda mrefu.
Makalla ametoa kauli hiyo leo mkoani Dar es Salaam wakati wa mwendelezo wa ziara ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za Wananchi ikiwemo migogoro ya ardhi ambapo leo ilikuwa zamu ya Jimbo la Mbagala.
Amesema baadhi ya Taasisi zinazomiliki maeneo hayo makubwa zimeyatelekeza kwa bila kuyaendeleza jambo linalosababisha wananchi kuingiwa na tamaa na kuweka makazi kutokana na uhaba wa maeneo.
Haya hivyo Makalla amezitaka Taasisi zote zinazomiliki maeneo makubwa ya ardhi kuhakikisha kuwa wanayaendeleza ikiwemo kuyawekea uzio ili kuondokana na uvamizi na kusababisha migogoro ya ardhi.

Wakati huo huo ameamuru kuondolewa kwa watu wote wanaofanya biashara ndani ya eneo la Ujenzi wa Barabara ya Mabasi yaendayo kasi kwa kuwa inamzuia mkandarasi kufanya majukumu yake.
Makalla amelazimika kutoa kauli hiyo kutokana na wafanyabiashara katika eneo la Mbagala Rangi Tatu kufanya biashara zao katika eneo la mradi huo licha ya ujenzi kuendelea.
Makalla ametoa agizo hilo leo Mbagala mkoani Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi katika majimbo yote akiwa na lengo la kuondoa migogoro hasa ya ardhi.
Amesema watu wanaofanya shughuli zao ndani ya eneo la mradi mbali na kumzuia Mkandarasi kufanya kazi zake pia wafanyabiashara hao wanahatarisha usalama wao.
Discussion about this post