UCHAFUZI wa Mazingira unaofikia viwango vya juu nchini India unaweza
kufupisha muda wa kuishi wa mamilioni ya watu kwa kipindi cha hadi miaka tisa.
Kulingana na taarifa za Shirika la Habari la CNN, utafiti uliochapishwa na
Chuo Kikuu cha Sera ya Nishati cha Chicago (EPIC) umebainisha kwamba idadi yote
ya Wahindi ambayo ni takriban bilioni 1.3 wanakabiliwa na kiwango hatari cha
uchafuzi wa mazingira unaozidi wastani wa uchafuzi uliowekwa na Shirika la Afya
Duniani (WHO).
Katika utafiti huo umeripotiwa kuwa uchafuzi wa hewa ulikuwa mbaya zaidi
katika Jimbo la Maharashtra eneo la Magharibi mwa Nchi na Madhya Pradesh
katikati mwa nchi.
Katika utafiti huo, imekadiriwa kuwa uchafuzi wa hewa, ambao umefikia
viwango vya hatari sana nchini India, unaweza kupunguza muda wa kuishi wa
mamilioni ya watu kwa kipindi cha hadi miaka tisa.
Utafiti huo, ambao umebainisha kuwa kiwango cha uchafuzi wa mazingira huko
New Delhi, Mji Mkuu wa India, pia uko juu zaidi,
Utafiti huo umeonesha kuwa kiwango cha uchafuzi wa hewa kinaweza kuongezeka
kwa matarajio ya maisha ya wakazi wa New Delhi hadi miaka 10, kadiri ukubwa wa
uchafuzi wa hewa unavyopungua kwa vigezo vya WHO.
Kulingana na utafiti wa EPIC, uchafuzi wa hewa nchini India unakadiriwa
kufupisha muda wa kuishi wa takriban watu milioni 520, ambayo inalingana na
asilimia 40 ya idadi ya watu nchini.
Awali kwa mujibu wa ripoti ya utafiti uliofanywa wa hali ya hewa duniani
‘State of Global Air 2020’ ambapo India na nchi zilizo kusini mwa jangwa la
Sahara barani Afrika zinaongoza.
Kwa mujibu wa utafiti huo, miongoni mwa watoto wadogo karibu 500,000
waliopoteza maisha chini ya mwezi mmoja baada ya kuzaliwa kutokana na uchafuzi
wa hali ya hewa mwaka jana, 116,000 mongoni mwao ni wa India, huku zaidi
ya vifo 236,000 vikiripotiwa katika nchi za chini ya jangwa la Sahara.
Kwa ujumla, waliofariki dunia kote duniani mwaka 2019 kutokana na uchafuzi
wa hali ya hewa kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na taasisi za Health
Effects Institute (HEI) na Institute for Health Metrics and Evaluation’s
Global Burden of Disease za Marekani, ni watu milioni 6.7
Discussion about this post