• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali kujenga Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji

by BAJETI
September 6, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI kupitia Sekta ya Uvuvi imeingia makubaliano na Chuo Kikuu cha Nelson Mandela pamoja na  Mfuko Kichocheo wa Kilimo Tanzania (TACT)  ili kujenga Kituo cha Ubunifu katika Uvuvi na tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji.

Lengo la ujenzi huo ni kusaidia kutatua changamoto za utafiti, ugani na ubunifu ili kuongeza tija katika Sekta hiyo nchini.

Akizungumza  wakati wa utiaji saini katika mkataba wa makubaliano hayo mwishoni mwa wiki  mkoani Kagera,Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, anayesimamia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah amesema kuwa kuanzishwa kwa Kituo hicho kutasaidia kutatua changamoto nyingi zinazokabili sekta ya Uvuvi na tasnia ya Ukuzaji Viumbe Maji.

“Napenda kuwaahidi wadau wote wa Sekta ya Uvuvi kuwa Wizara itaendelea kuunga mkono juhudi za wavuvi, Wakuzaji Viumbe Maji, Wachakataji, na Wafanyabiashara wa bidhaa za Uvuvi ili ziweze kuwa na tija na kuleta ustawi wa wadau wote nchini,”  amesema Dkt. Tamatamah

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji, Mfuko Kichocheo wa Kilimo Tanzania, Dkt. John Kyaruzi amesema wameamua kuwekeza katika utafiti kwenye Sekta ya Uvuvi ili iweze kuwa endelevu na kuwasaidia wawekezaji kuwa na taarifa za msingi zitakazowasaidia kuwekeza kwa tija ili kuimarisha biashara zao.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali, Charles Mbuge amewataka Viongozi wa Mkoa huo kuupokea mradi huo kwa kuwa hiyo ni neema iliyowafikia katika eneo lao.

Amesema kuwa viongozi hao hawana budi kukusimamia mradi huo  unafanikiwa ili uweze kuleta tija kwa jamii hususani vijana ili waweze kujiajiri kupitia shughuli za uvuvi na kukuza uchumi wao na wa nchi pia.

“Halmashauri zetu mpo hapa pamoja na Viongozi, naomba suala hili mlitilie maanani, uwekezaji huu ukifanikiwa hapa kwetu utasaidia kujenga uchumi wa Mwananchi mmoja mmoja hadi Taifa kwa ujumla,” amesema  Meja Jenerali Mbuge

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, Prof. Emmanuel Luoga amebainisha kuwa nia ya Chuo hicho ni kufanya tafiti zitakazotoa matokeo chanya kiuchumi na kiikolojia ili kufanya shughuli za uvuvi kuwa endelevu.

Mkurugenzi Mtendaji, Mfuko Kichocheo wa Kilimo Tanzania(TACT), Dkt. John Kyaruzi (wa kwanza kulia)  akiwa na Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah,Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Prof. Faustine Kamuzora (wa tatu kulia) na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, Prof. Emmanuel Luoga (wa kwanza kushoto) wakionesha mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa Kituo  cha utafiti na Ukuzaji Viumbe Maji  mara baada ya kuweka saini  mkoani Kagera hivi karibuni(Picha na mpigapicha wetu)

Katika sehemu ya makubaliano hayo Wizara imepanga kufanya tathmini ya  mazingira na kurekebisha sera na sheria zote ambazo kwa namna moja au nyingine zimekuwa kikwazo kwa shughuli za uvuvi.

Chuo Cha Nelson Mandela kitajikita kufanya tafiti tumizi ili kusaidia Sekta ya Uvuvi na wadau wake kuwa na taarifa sahihi zitazowasaidia kuboresha shughuli zao na Mfuko Kichocheo wa Kilimo (TACT) watawekeza mitaji ili kuchachua uwekezaji katika Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji nchini.

Next Post

Watakiwa kutumia njia za asili kukabiliana na wanyamapori

Sensa yaibua Vikwazo Sekta ya Kilimo

DC aagiza kutengwa siku kusikiliza kero za wananchi.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In