• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

DC aagiza kutengwa siku kusikiliza kero za wananchi.

by BAJETI
September 7, 2021
in Habari
0
Share on FacebookShare on Twitter

MKUU wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Mhandisi Richard Ruyango amewaagiza Viongozi wa Halmashauri  ya Wilaya ya Meru kutenga  siku ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wilayani humo.

Ruyango ameyasema hayo wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kilichokutana mwishoni mwa wiki iliyopita huku madiwani wakiwasilisha taarifa za Kata zao katika kipindi cha Aprili hadi June 2021.

Mhandisi Ruyango amesema ni muhimu kwa viongozi wa ngazi zote katika wilayani humo kuwa na siku moja kwa ajili ya kusikiliza matatizo ya wananchi ambapo wengine yanaweza kutatuliwa bila kufikishwa ngazi za juu zaidi hivyo kupunguza kero zo.

“Viongozi  kuanzia ngazi za Kitongoji, Vijiji, Kata na Wilaya kutenga siku ya Jumanne kusikiliza  na kutatua kero za wananchi .

“Si vyema mwananchi ana kero ambayo inaweza kutatuliwa na Viongozi wa eneo lake, atumie nauli na muda wake kuja ngazi za Wilaya” amesema Ruyango

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru  Zainabu Makwinya amesema ni muhimu kwa  Watumishi wote wa Halmashauri hiyo kusikiliza kero za wananchi kwa wakati sambamba na kutoa sababu za msingi kwa kero ambazo zinazohitaji muda.

“Maafisa Utumishi wa ngazi za Vijiji na Kata wanatakiwa kufanya uchunguzi na kutoa takwimu sahihi za  wanafunzi ambao hawajaripoti shule”amesema Makwinya

Amesema kuwa maafisa Utumishi  wanapaswa kufuatilia kwa karibu zaidi na kutoa taarifa sahihi kwa Maafisa Elimu kuhusu idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari na wale ambao hawajaripoti.

Diwani wa Kata ya Imabaeny ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru mkoani Arusha Jeremiah Kishili akichangia mada katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita(Picha na mpigapicha wetu)

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo  Jeremiah Kishili  amesema mbali na changamoto nyingine zilizopo katika Sekta ya Elimu ni muhimu kuwepo na utaratibu ambao utasaidia Walimu wanaopangiwa kazi  katika shule za vijijini kutopata uhamisho.

Amefafanua kuwa Walimu wasipate uhamisho  usiokuwa na sababu za msingi kwa kuwa shule za vijijini zinazokabiliwa na upungufu wa Walimu.

Kishili ambaye ni Diwani wa Kata ya Imabaeny ameongeza kuwa  Walimu wengi wanapopangiwa kufanya kazi katika shule za vijijini wamekuwa wakihama muda mfupi   baada ya kuripoti kutokana na changamoto ndogo ndogo za kimazingira.

Amebainisha kuwa hali hiyo ya walimu kuhama inachangia wanafunzi kushindwa kufanya vizuri katika  masomo yao.

Naye Ofisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo Anjela Urassa amesema tayari wamekwishaandaa  ripoti ya wanafunzi ambao hawajaripoti shule.

Amesema ni muhimu pia kwa Viongozi wa Vijiji na Kata kuelewa zaidi na kufahamu makazi ya wazazi wa  wanafunzi   na mazingira waliopo watoto hao ili kisaidia ufumbuzi wake.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya hiyo Mhandishi Richard Ruyango hayupo pichani wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika wilayani humo mwishoni mwa wiki(Picha na mpigapicha wetu)
Next Post

Washerekea wafungwa kutoroka gerezani

Wakulima wakwepa mbolea ya viwandani

Watu tisa kati ya 10 hupumua hewa iliyochafuliwa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In