• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Watu tisa kati ya 10 hupumua hewa iliyochafuliwa

by BAJETI
September 8, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonya kuwa watu 9 kati ya 10 wanapumua hewa iliyochafuliwa, hali ambayo kila mwaka inasababisha vifo vya mapema vya watu milioni 7.

Amesema kati ya hao  watoto ni 600,000  na kuhimiza kuchukuliwa hatua madhubuti kutatua changamoto hiyo sasa ili kuzuia idadi  ya vifo isiongeze ifikapo mwaka 2050. 

Guterres ametoa kauli hiyo jijini New York nchini Marekani wakati wa maadhimisho ya Siku ya Hewa Safi na Anga ya Bluu ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Septemba 9.

Hata hivyo Guterres katika taarifa yake amekumbusha kuwa uchafuzi wa hali ya hewa ni “dhihirisho la wazi la ukosefu wa usawa ulimwenguni,” kwani vifo vingi vinavyohusiana na janga hili hufanyika katika nchi za kipato cha chini na cha na kati na katika vitongoji masikini vya mataifa tajiri.

 “Umaskini unalazimisha watu kuishi karibu na vyanzo vya uchafuzi wa mazingira, kama vile viwanda na barabara na pia husababisha watu Bilioni tatu wanaendelea kutumia mafuta kisukuku au mafuta ya taa kwa kupikia na kwa kupasha nyumba joto na kuwasha taa”amebainisha Guterres. 

Aidha amefafanua kuwa uchafuzi wa mazingira sio tu unaharibu afya za binadamu, lakini pia unachangia kuongeza shida ya hali ya hewa,

“Katika siku hii ya kimataifa ya hewa safi kwa anga ya bluu, ninahimiza nchi zote kufanya bidi zaidi ili kuboresha hali ya hewa na Sheria ya kitaifa inayotegemea ushahidi inaweza kusaidia kutekeleza miongozo juu ya ubora wa hewa iliyowekwa na Shirika la afya duniani”ameeleza Guterres.

Wakati huo huo, Guterres ametaka kuwe na viwango vikali vya kudhibi kuchafua hewa kunakotokana na magari, mitambo, ujenzi na viwanda, kuondoa matumizi ya makaa ya mawe na kuwekeza katika nishati mbadala badala ya mafuta kisukuku(mafuta ya taa). 

“Ikiwa tutachukua hatua hizi, tunaweza kuokoa hadi maisha ya watu milioni 150 katika karne hii na kusaidia kusafisha mazingira yetu,” ameongeza Guterres

Next Post

Jeshi lawaachia wafungwa wa kisiasa

Serikali kuwapatia makazi Kaya 644 Magomeni Kota

Nyota Klabu ya Simba kuibua vipaji Segerea

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In