KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, gari lililobeba aina mpya ya chanjo ya ugonjwa wa UVIKO-19(CORONA) limeshambuliwa na kisha wezi kuiba dozi za chanjo hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Habari la TRT imeeleza kuwa gari lililobeba chanjo za (UVIKO-19)CORONA lilishambuliwa baada ya kutoka kwenye ghala la Wizara ya Afya ya nchi hiyo katika Mkoa wa Yaftabad.
Washambuliaji walilishambulia gari hilo jijini Tehran, Mji Mkuu wa Iran na kisha kuiba dozi 300 za chanjo ya UVIKO-19, baada ya kumpiga dereva wa gari.
Mkuu wa Polisi wa Tehran Husein Rahimi amesema kuwa juhudi zinaendelea kuwakamata wezi hao.
Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Umma wa Wizara ya Afya ya nchi hiyo Kiyanuş Cihanpur amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Discussion about this post