MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla anatarajiwa kuanza kusikiliza na kutatua kero za Wananchi wa Mkoa Dar es Salaam wakiwemo wale wenye migogoro ya ardhi.
Hiyo ni sehemu ya mkakati wake wa kuhakikisha kuwa anatataua kero za wananchi katika majimbo yote ya Mkoa wa Dar es Salaam zikiwemo zile za migogoro sugu ya ardhi na kuahidi kila mtu atapata haki yake kwa mujibu wa Sheria.
Makalla ameyasema hayo leo Agosti 26,mkoani Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya mikakati ya kuufanya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa wa kisasa ikiwemo usafi.
Amesema ziara hiyo itaanza rasmi Agosti 30,2021 Jimbo la Kawe ambapo Agosti 31 atakuwa Jimbo la Kibamba.
Aidha amebainisha kuwa September mosi,2021 atakuwa Jimbo la Segerea,September 2 Jimbo la Mbagala na September 3 Jimbo la Kigamboni ambapo zoezi hilo litaanza kuanzia saa mbili asubuhi hadi majira ya jioni.
Hata hivyo Makalla ameongeza kuwa atafuatana na jopo la wataalamu wakiwemo Watendaji wa Serikali, Wanasheria, Kamishna wa Ardhi, Maafisa Ardhi, Jeshi la Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) na wadau wote wanaojihusisha na masuala ya kisheria. Wananchi wote wenye migogoro wameombwa kutumia fursa hiyo kuwasilisha malalamiko yao ili yaweze kupatiwa ufumbuzi kwa mujibu wa Sheria

Discussion about this post