HALMASHAURI ya Jiji la Arusha imepanga kukusanya zaidi ya Sh.Bilioni 24 kwa Mwaka wa Fedha 2021 /2022 ambapo asilimia 60 ya fedha hizo zitaenda katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni jijini Arusha na Mstahiki Meya wa jiji hilo, Maxmilian Iranghe wakati akizungumza katika kikao cha mwisho cha Baraza la Madiwani kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021.
Amesema katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 kwenye malengo ya kibajeti wanatarajia kupata kiasi hicho cha zaidi ya Sh.Bilioni 24 ambapo baadhi watazipeleka kwenye miradi ya maendeleo ikiwemo ya Elimu.
Iranghe ameongeza kuwa kwa upande wa mipango miji wamejitahidi kutoa vibali vya ujenzi kwani wanahitaji Arusha inayokuwa kwa kasi na ijengwa kisasa zaidi.
Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji hilo Dkt John Pima amewataka wananchi kuzingatia ujenzi wa mipango miji kwa kuwa kufanya hivyo kutasaidia kutatua baadhi ya kero zinazoweza kujitokeza dhidi yao.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji, Ujenzi na Mazingira ya jiji hilo ambae pia ni Diwani wa Kata ya lemara Nabot Silas amefafanuwa kuwa wameweka mikakati mingi ya ujenzi katika jiji lao.
Hata hivyo amewataka wananchi kutoharibu miundombinu mbinu kwani wamekuwa wakizuia malengo halisi yaliyowekwa kwa ajili ya miundombinu hiyo.
Discussion about this post