WAZAZI nchini wametakiwa kushirikiana na Walimu na wakiwemo walezi wengine wa Shule kuhakikisha kuwa watoto wanafanya vizuri na kutimiza malengo waliyojiwekea katika elimu.
Mbali na hilo lakini pia Walimu wametakiwa kuwapeleka wanafunzi katika mitihani ya ujirani mwema ili kuwajengea uwezo wa kufanya vizuri katika masomo yao.
Akizungumza katika mahafali ya Tano ya Darasa la Saba katika Shule ya Msingi Tumaini Mistion iliyopo wilayani Arumeru Mkoa wa Arusha, Mkurugenzi wa Shule ya Msingi Mecsons Mecky Shirima amesema ni muhimu kwa Wazazi kushirikiana na Walimu kwa kuwa jambo hilo hutengeneza mazingira mazuri baina ya pande hizo mbili hali inayosaidia wanafunzi kufanya vizuri.
Amesema ni muhimu kwa Walimu pia kuwapeleka wanafunzi katika mitihani ya ujirani mwema ili kuwajengea uwezo wa kufanya vizuri katika masomo yao.
Amesema kufanyika hivyo kunajenga uwezo kwa mwanafunzi kujiamini katika kufanya mitihani yake ya mwisho hali inayoongeza ufauli zaidi.
Hata hivyo Shirima amewataka wahitimu kutambua kuwa Elimu haina mwisho hivyo wanapaswa kusoma kwa bidii kutokana na kukuwa kwa Sayansi na Teknolojia.

Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Namnyaki Mollel amesema wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakifanya mitihani ya ujirani mwema ambayo wamekuwa wakifanya kwa shule zilizopo ndani ya mkoa na hata nje ya Mkoa wa Arusha.
Amesema kuwa shule hiyo inatarajia kuanzisha Sekondari pamoja na vyuo vya ufundi kwa faida za vizazi vijavyo.
Mwalimu Namnyaki amewasihi wahitimu hao kutojihusisha na makundi yeyote mabaya ambayo yatazima ndoto zao katika elimu na badala yake wawe mabalozi Waziri ndani ya jamii.
Discussion about this post