• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Nyoka wasababisha vifo vya watu 137,000

by BAJETI
September 15, 2021
in Mazingira
0
Share on FacebookShare on Twitter

IDADI ya watu wanaopoteza maisha kila mwaka kutokana na athari zinazosababishwa na kuumwa na nyoka wenye sumu imefikia zaidi ya 137,000 huku wengine wakipata ulemavu.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO) wakati wa uzinduzi wa jukwaa maalum mtandaoni kwa lengo la kutoa taarifa na kuelimisha umma kuhusu hatari ya kuumwa na nyoka wenye sumu na nyoka wapi waliko nyoka hao hatari zaidi duniani mjini Geneva,Uswisi.

Shirika hilo limesema watu 81,000 hadi 137,000  hufariki dunia kutokana na athari zinazosababishwa na kuumwa na nyoka wenye sumu ingawa idadi kamili ya walioumwa na nyoka hadi sasa haijulikani.

Hata hivyo kwa mujibu wa WHO makadirio yanaonesha kuwa takriban watu Milioni 5.4 huumwa na nyoka kila mwaka huku Milioni 2.7 kati yao huumwa na nyoka wenye sumu kali ambao husababisha athari mbaya kwa mamilioni ya maisha ya watu na wengi wao wakiwa masikini.

Mbali ya vifo vya watu 137,000 kila mwaka, kuumwa na nyoka pia kumewaacha mamilioni ya watu na ulemavu wa maisha

WHO imebainisha kuwa kuumwa na nyoka mwenye sumu kali kunaweza kusababisha kupooza ambako kunaweza kumzuia mtu kupumua, kumsababishia maradhi ya kutokwa na damu, matatizo ya figo yasiyoweza kutibika na kuharibu mishipa ambayo inapelekea ulemavu wa maisha na kukatwa viungo. 

Shirika hilo limeongeza kuwa kuumwa na nyoka ni moja ya magonjwa yaliyopuuzwa NTDs  ambayo athari zake ni kubwa na mbaya kuliko inavyodhaniwa.  

WHO imebainisha kuwa waathirika wakubwa ni watu wanaofanya kazi katika Sekta ya Kilimo na Watoto huku maeneo yaliyoathirika na kuwa hatarini zaidi ni Afrika, Asia na Amerika ya Kusini katika maeneo ya Vijijini  

“Mathalani barani Asia watu wapatao milioni 2 hudhurika na sumu ya nyoka kila mwaka na Afrika watu 435,000 hadi 580,000 huhitaji matibabu kila mwaka baada ya kuumwa na nyoka. 

“Ili kupunguza idadi ya vifo na ulemavu utokanao na kuumwa na nyoka ni lazima kuziwezesha na kuzishirikisha jamii, pili kuhakikisha kuna matibabu salama na yenye ufanisi, tatu kuimarisha mifumo ya afya na nne kuongeza ushirika, uratibu na rasilimali za kupambana na zahma hii”imefafanua taarifa hiyo. 

Next Post

Serikali yataka uhuru wa kisera kwa nchi zinazoendelea

Wanawake waongoza kumiliki silaha Marekani

Wanawake waongoza kumiliki silaha Marekani

TAIWAN kuipatia Japan mitungi 1000 ya gesi kupambana na UVIKO-19

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In