ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Meru Elias Kitoi amewataka watanzania na waumini wa madhebebu ya Kikristo kuheshimu muda ili kujipatia maendeleo.
Askofu Kitoi ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 12 wa Jimbo la Kati lilipo katika Dayosisi ya Meru mkoani Arusha uliofanyika katika Usharika wa Makumira wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Amesema muda ni kitu kichobadilisha dunia na watu wanapata mali kutokana na kutumia muda wao vizuri lakini kuna watu wengine wanakwenda kwa manabii ili kupata mali wakati wameshindwa kutumia muda wao vizuri..
Amebainisha kuwa kila mkristo anapaswa kuwa wakili mzuri wa muda wakati wote huku akisisitiza kuwa kumtumikia Mungu ni kitu rahisi na sio kitu cha kushikika wala kuonekana
Kwa upande wake Mkuu wa Jimbo la Kati Mchungaji Abel Kaaya amewaasa Vijana kuzitafuta fursa ili ziweze kuwaletea maendeleo yao binafsi ikiwa ni pamoja na kutumia muda vizuri.
“Mkutano huu wa 12 tutajadili na kufanya tathimini ya mambo mbalimbali yaliyofanyika katika kipindi cha miaka miwili iliyopita”amesema Mchungaji Kaaya
Naye Mwalimu Lightness Marko ambaye anamaliza muda wake wa uongozi katika Jimbo hilo ametoa wito kwa viongozi watakao patikana kuifanya kazi ya Mungu kwa bidii bila kuchoka ili kuleta amani na upendo katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Discussion about this post