WAZAZI wametakiwa kuacha kuwashawishi watoto wao kusomea fani wasizozipenda na badala yake wawape uhuru wa kusoma kile kilichopo katika ndoto zao.
Kauli hiyo imetolewa leo wilayani Arumeru Mkoa wa Arusha na Mchungaji kutoka nchini Kenya wa Kanisa la Saimoni Nzuwa wakati wa mahafali ya 12 ya darasa la saba katika Shule ya Haradali ambapo wanafunzi 115 wamehitimu.
Amesema baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwashinikiza watoto wao kusoma fani wasizozipenda jambo ambalo linakwamisha mafanikio ya wanafunzi katika kutimiza ndoto zao.
Pamoja na hayo Nzuwa amewataka wahitimu hao kumcha Mungu Halisi na kuacha kujihusisha na makundi ya anasa
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Aidan Rwakabuga amesema pamoja na shule hiyo kuongeza kiwango cha ufaulu kila mwaka lakini bado wanakabiliwa na upungufu wa vitabu vya kiada na ziada
Hata hivyo amewataka wanafunzi hao wanaohitimu darasa la saba kuendelea kujituma katika kusoma licha ya kufanya kazi za nyumbani
“Tunawaomba wazazi kuhakikisha kuwa wanafuatilia mienendo ya watoto ili kuepuka sababu mbalimbali zinazoweza kuwakwamisha kujiunga na Elimu ya Sekondari”amesema Mwalimu Rwakabula


Discussion about this post