• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Nderiananga:Wafichueni watoto wenye ulemavu wa kusikia

by BAJETI
September 21, 2021
in Habari
0
Share on FacebookShare on Twitter

SERIKALI imeitaka jamii nchini  kuacha kuwaficha na badala yake kuwafichua watoto wenye ulemavu wa kusikia (Viziwi)kwa kuwa wana haki ya kupata elimu sawa na watoto wengine  wasiona na ulemavu

Mbali na ulemavu huo lakini pia watoto hao wana uwezo wa kufanya vizuri  hata zaidi ya watoto ambao hawana ulemavu wa kusikia.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Arusha na Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika na Walemavu  Ummy Nderiananga katika mahafali ya kwanza ya kidato cha nne katika  Shule ya Wanafunzi wenye Ulemavu wa Kusikia ya Shirika la Roho Mtakatifu na  mahafali ya 14 ya Shule Sekondari ya Wavulana Tengeru.

Amesema kuwa jamii inapaswa kuachana na dhana ya kuwaficha nyumbani watoto wenye ulemavu  wa kusikia badala Yake wawafichue na kuwapeleka shuleni kwa kuwa nao wana haki ya kupatiwa elimu bora kama walivyo watoto wengine kwenye jamii.

Hata hivyo Nderinanga amefurahishwa na jitihada  nzuri zinazofanywa  na watoto wenye ulemavu wa kusikia(viziwi) katika elimu ambapo wengi wameonesha kufanya vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shule ya wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia  Padri John Asei ameiomba serikali kuwa na mitaala ambayo inahusisha watoto wenye ulemavu kuanzia elimu ya awali mpaka chuo kikuu ili kuwawezesha kupata elimu bora.

Naye Mkuu wa Shule ya  Sekondari  ya Wavulana Tengeru Mwalimu  Gaudens  Mtui amesema  kuwa shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri kutokana na maadili mema ambayo wamekuwa wakifundishwa kwani tangu kuanzishwa kwake hakuna mwanafunzi aliyewahi kupata ufaulu wa alama sifuri.

Hata hivyo Mtui amebainisha kwamba  wanatarajia wanafunzi wa shule hizo kuweza kufanya vizuri zaidi katika mitihani  ya kuhitimu kidato cha nne ikiwa na wahitimu 126 kidato cha nne huku wanafunzi wanaohitimu katika shule ya ulemavu wa kusikia  wakiwa saba.

Next Post

Kampeni ya changia damu kuokoa maisha yaanza kwa kishindo

TRC yasafirisha tani 800 za mbolea kuelekea Kigoma

TRC yasafirisha tani 800 za mbolea kuelekea Kigoma

Mtambo achangia ujenzi Zahanati ya Kijiji Dondo

Mtambo achangia ujenzi Zahanati ya Kijiji Dondo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In