• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Sayansi na Teknolojia

Kampeni ya changia damu kuokoa maisha yaanza kwa kishindo

by bajeti
November 14, 2021
in Sayansi na Teknolojia
0
Share on FacebookShare on Twitter

MPANGO wa Taifa wa Damu Salama nchini umezindua kampeni ya kitaifa ya kuihamasisha jamii kuchangia damu ili kuokoa vifo kwa akina mama wajawazito vinavyotokana na uzazi.

Kampeni hiyo inakuja kutokana na kile kinachoelezwa kuwa vifo vingi vya akinamama wajawazito vilisababishwa  na kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua hivyo ni jukumu la jamii yote kuchangia damu ili kuokoa vifo hivyo.

Akizungumzia Kampeni hiyo Septemba 20,2021 jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Idara ya Ukusanyaji Damu katika Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Dk. Avelina Mgasa amesema kauli mbiu ya kampeni za mwaka huu wa 2021 ni “Changia Damu Kuokoa Wanaoleta Uhai Duniani”.

“Kampeni hii inalenga kuihamasisha jamii kujitolea kutoa damu kwa hiyari ili kuokoa maisha ya kina mama wajawazito ambao wanatumika kama chombo cha kuleta uhai duniani” amesema Dk. Mgasa

Maabara inayotumika kuhifadhia damu na kuipima kabla ya kuruhusiwa kutumika kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu(Picha na mpigapicha wetu)

Dk.Mgasa amefafanua kuwa Kauli mbiu inatupa hamasa na kuihamasisha jamii kujitolea kuchangia damu kwa hiari ili kuongeza upatikanaji wa damu ya kutosha na salama ambayo itasaidia kuokoa maisha ya kina mama ambao hupoteza maisha kila siku kutokana na matatizo ya uzazi na wakati wa kujifungua.

Ameongeza kuwa Kampeni hiyo iliyozinduliwa katika Kanda zote saba za kukusanya damu nchini imeanza siku ya Jumatatu ya Septemba 20,2021 na imelenga kukusanya chupa za damu 19,514 kutoka kwenye timu 226 zilizopo nchi nzima ambazo ni asilimia tatu ya malengo yao ya damu kwa mwaka.

Aidha Dk. Mgasa ameongeza kuwa Kampeni ya mwaka huu inailenga jamii kuwa wachangiaji wa damu kwa kuwa asilimia 80 ya damu inayokusanywa nchini, inakusanywa kutoka kwa wanafunzi na vijana wanapokuwa shule za sekondari na vyuoni.

Mkuu wa Idara ya Ukusanyaji Damu katika Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Dk. Avelina Mgasa akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) mkoani Dar es Salaam hivi karibuni jinsi Damu salama inavyohifadhiwa tayari kwa matumizi ya binadamu(Picha na mpigapicha wetu)

Next Post
TRC yasafirisha tani 800 za mbolea kuelekea Kigoma

TRC yasafirisha tani 800 za mbolea kuelekea Kigoma

Mtambo achangia ujenzi Zahanati ya Kijiji Dondo

Mtambo achangia ujenzi Zahanati ya Kijiji Dondo

Watu bilioni 2.6 hawana fursa kupata nishati safi ya kupikia

Watu bilioni 2.6 hawana fursa kupata nishati safi ya kupikia

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In