KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema zaidi ya watu Milioni 760 wanakosa fursa ya nishati ya umeme huku wengine Bilioni 2.6 bado hawana fursa ya kupata nishati safi ya kupikia.
Guterres ameyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa ngazi ya juu kuhusu nishati unaofanyika kandoni mwa mjadala mkuu wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ambao leo umeingia katika siku ya nne
Amefafanua kuwa ni miaka 40 sasa tangu suala la nishati lilipojadiliwa katika mkutano wa ngazi ya juu, na leo hii dunia inakabiliwa na ukweli kwamba karibu watu milioni 760 bado wanakosa fursa ya nishati ya umeme.
“Jinsi tunavyozalisha na kutumia nishati ni chanzo kikuu cha mgogoro wa mabadiliko ya tabianchi, hewa chafuzi itokanayo na nishati ni takribani asilimia 75 ya gesi yote chafuzi ya viwandani.”
“Tuna umuhimu mara mbili wa kumaliza umaskini wa nishati na kupunguza mabadiliko ya tabianchi, na tuna jibu ambalo litatimiza maagizo yote mawili, nishati nafuu, mbadala na endelevu kwa wote na hili ndilo lengo na ni lengo la maendeleo endelevu namba saba.”amesema Guterres
Guterres amesisitiza kuwa kuwekeza katika nishati safi, ya bei rahisi kwa wote kutaboresha ustawi wa mabilioni ya watu na kunaweza kuunda ajira zinazojali mazingira.
“Tunahitaji haraka ili kujikwamua na janga la ugonjwa wa UVIKO-19 na pia kutasongesha malengo yote ya maendeleo endelevu na ni suluhisho moja muhimu zaidi la kuepusha janga la mabadiliko ya tabianchi”Amesema Guterres




Discussion about this post