• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Friday, May 15, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Tani 24 za zebaki hutumika kuchenjulia dhahabu

by bajeti
March 17, 2023
in Mazingira
0
Serikali  yaandaa mpango-kazi kuondoa matumizi  ya  Zebaki

Wachimbaji wadogo wa dhahabu katika mgodi wa Chikoa uliopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma wakiwasikiliza maofisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira kuhusu athari za matumizi ya zebaki kwa afya na mazingira hivi karibuni (Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

TANI 24 za kemikali hatari ya Zebaki hutumika kwa mwaka katika shughuli za uchenjuaji wa dhahabu nchini ambapo wachimbaji wadogo   ndio watumiaji wakubwa.

Hayo yamebainishwa katika Mpango-Kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu kwa mwaka 2020-2025 ulioandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira.

Mpango huo umekuja baada ya Jumuia ya Kimataifa mnamo mwaka 2013 kupitisha Mkataba wa MINAMATA  wenye madhumuni ya kulinda afya ya binadamu dhidi ya madhara ya uchafuzi wa mazingira unaotokana na Zebaki.

Hata hivyo kutokana na serikali kuona umuhimu wa kulinda afya za watanzania na mazingira kwa ujumla iliuridhia mkataba huo na kuusaini mwaka 2020.

Mpango-Kazi huo umefafanua kuwa wachimbaji wadogo huchenjua dhababu kwa kutumia mbinu ambazo huhatarisha afya za binadamu na mazingira.

“Shughuli za wachimbaji wadogo wa dhahabu zimekuwepo nchini kwa zaidi ya miaka 100 huku tathmini ikionesha kuwa takribani tani 13.2 hadi 24.4 za Zebaki hutumika kwa mwaka katika shughuli za uchenjuaji wa dhahabu.

“Uchomaji holela wa dhahabu,uchenjuaji wa dhahabu karibu na maeneo ya makazi na vyanzo vya maji na uchenjuaji wa marudio yenye Zebaki kwa kutumia sayanadi kunakochangia zaidi uchafuzi wa mazingira”umefafanua Mpango Kazi huo.

Zebaki ikionekana kabla ya kutumika kuchenjulia dhahabu(Picha na Goodluck Hongo)

Hata hivyo lengo la Mpango-Kazi huo ni kupunguza na pale inawezekana kuondosha matumizi ya Zebaki katika shughuli za Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu ili kulinda afya za wananchi na mazingira

Kwa mujibu wa Mpango-Kazi huo umebainisha kuwa,Shirika la Afya Duniani (WHO) limeitaja Zebaki kuwa ni miongoni mwa vyanzo 10 hatarishi kwa afya ya binadamu duniani.

Awali akizungumza na waandishi wa habari kutoka Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira (JET) kuhusu madhara ya zebaki,kwa mazingira na afya za binadamu Mratibu wa Mradi wa EHPMP  kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Mhandisi Benjamin Mchwampaka amesema Zebaki ikiingia mwilini husababisha magonjwa ambayo kwa ujumla yanajulikana kama MINAMATA.

“MINAMATA huathiri Mfumo wa Neva na kusababisha magonjwa kama miguu na mikono kufa ganzi na kukosa nguvu, misuli kulegea, figo kuathirika, uono hafifu, kupoteza uwezo wa kusikia na kuongea,mimba kuharibika, kuzaa watoto wenye matatizo ya akili au wenye viungo pungufu, kupoteza kumbukumbu, kukosa usingizi kwa muda mrefu, kiharusi na hatimaye kifo”.

“Kutokana na athari hizo,MINAMATA inarithishwa kutoka kizazi hadi kizazi”amefafanua Mhandisi Mchwampaka

 

Mchwampaka amesema serikali inaendelea kuchukua hatua dhidi ya matumizi ya zebaki ikiwemo kupatikana kwa teknolojia mbadala ili kuchana na matumizi ya zebaki katika shughuli za uchejuaji wa dhahabu na kutoa elimu kwa wahusika ili kulinda mazingira na afya zao.

Kwa mujibu wa Mkataba wa MINAMATA unazitaka Serikali ambazo ni wanachama wa mkataba huo zitawajibika kisheria kuchukua hatua mbalimbali kushughulikia athari za Zebaki katika maisha yao yote”amesema Mchwampaka

Hatua hizo ni pamoja na kupiga marufuku madini mapya ya Zebaki,kutokomeza yaliyopo na kusimamia matumizi ya Zebaki katika uchimbaji mdogo wa madini  ya dhahabu,michakato ya utengenezaji na uzalishaji wa vitu vya kila siku kama vile vipodozi,balbu,betri na unga unaotumika kujaza meno.

Next Post
SMT:Mshirikiane na serikali  kuzuia uharibifu wa mazingira

SMT:Mshirikiane na serikali  kuzuia uharibifu wa mazingira

Majengo kuwekewa mfumo wa umeme kuchajisha magari

Majengo kuwekewa mfumo wa umeme kuchajisha magari

Sea Sense pelekeni elimu Pemba kuwalinda Kasa

Sea Sense pelekeni elimu Pemba kuwalinda Kasa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:21
  • Today's page views 22
  • Total visitors 16,236
  • Total page views 18,409

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In