• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Sea Sense pelekeni elimu Pemba kuwalinda Kasa

Kasa sio samaki

by bajeti
December 2, 2021
in Mazingira
0
Sea Sense pelekeni elimu Pemba kuwalinda Kasa

Ofisa Uvuvi Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga Ezra Katete (kushoto) akiwaonesha maofisa kutoka Shirika lisilo la kiserikali la Sea Sense gamba la kasa aliyevuliwa na nyama yake kuliwa katika ufukwe wa bahari ya hindi mkoani humo(Picha na Maktaba)

Share on FacebookShare on Twitter

NOVEMBA 28,2021 vyombo ,mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi vilitoa taarifa ya vifo vya watu saba na wengine 24 kulazwa hospitali baada ya kudaiwa kula nyama ya Kasa huko Pemba Zanzibar.

Hata hivyo kwa Zanzibar hilo sio tukio la kwanza ambapo Januari,2012,watu wa familia moja walifariki dunia katika Kijiji cha Tumbe Wilaya ya Micheweni Pemba na wengine sita kulazwa hospitali wakiwa katika hali mbaya baada ya kudaiwa kula nyama ya kasa.

Kasa huyo alivuliwa kutoka baharini Januari 3,2012 ambapo baada ya kuchinjwa alitengezezwa na nyama yake kupelekwa  nyumbani kwa ajili ya kitoweo.

Baada ya familia kula nyama hiyo, iliwachukua saa 3 kuanza kupata athari za nyama yake kwa kuugua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, wa wakati huo Yahya Rashid Hemed alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi waache ukaidi wa kula nyama ya kasa.

Amesema wananchi wakiendelea na ukaidi kwa maagizo yanayotolewa ndipo madhara yanapojitokeza jambo ambalo huathiri jamii.

Katika eneo la Pemba kunahitajika elimu kutoka kwa watalaamu ili kusaidia kufafanua  umuhimu wa kuwalinda kasa na madhara yake kwa binadamu.

Baadhi ya wananchi wa Wilaya la Mkinga mkoani Tanga wakiwa katika mkutano hadhara wakipata elimu ya kulinda mazingira ya habari na kuacha kula nyama ya kasa na mayai yake kutokana na sumu aliyonayo  kiumbe huyo kutoka kwa viongozi wa Shirika lisilo la kiserikali la Sea Sense (Picha na Maktaba)

Kwa Tanzania Bara Shirika lisilo la kiserikali la Sea Sense limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu juu ya kulindwa kwa mazingira ya bahari na umuhimu wa kumlinda kasa na athari zake kwa binadamu pindi nyama yake ikiliwa na binadamu

Sea sense walianza kazi ya kuhamasisha kulindwa kwa mazingira ya bahari tangu miaka ya 2000 wakianzia na Wilaya ya Mafia mkoani Pwani na baadaye kuhamia katika wilaya zingine za Mkuranga na Kibiti.

Wilaya zingine ambazo Shirika hilo lilifanya kazi ya kulinda uvuliwaji wa kasa ni pamoja na  Mkinga,Pangani,Tanga jiji na Muheza mkoani Tanga  pamoja na Kigamboni mkoani Dar es Salaam  na Kilwa Mkoa wa Lindi.

Katika maeneo hayo wananchi wengi wanaelewa madhara ya kula nyama ya Kasa hivyo kupunguza athari za kiumbe huyo anayeonekana kupendwa na jamii za watu wa mwambao wa bahari.

Shirika hilo lilifanikiwa kutengeneza mfumo wa maafisa Kasa zaidi ya 38 katika  wilaya hizo ili kudhibiti uvuliwaji na ulaji wa nyama ya kasa ikiwemo mayai yake ambao wananchi kutoa taarifa za siri pindi wanapoona kavuliwa au kusambazwa kwa nyama yake.

Akizungumzia hali hiyo mkoani Dar es Salaam leo,mtaalamu wa masuala ya mazingira na viumbe wa baharini Omary Mapoy amesema kuna Kasa wa aina saba lakini Tanzania wapo wa aina tano pekee ambapo ni Kasa Kawaida,Ng’amba,Duvi,Kigome na Noa

Amesema aina mbili zilizobaki za kasa hupatikana katika nchi zenye baridi kali na huweza kukua hadi kufikia uzito wa tani moja lakini kasa sio samaki kama wetu wanavyodhani bali ni moja kati ya viumbe vinavyoishi majini na majike hutoka nchi kavu kwa ajili ya kutaga mayai na kisha kurudi baharini kuendelea na maisha yao.

“Kasa wana madhara makubwa kwa binadamu na kupelekea vifo kwa sababu wanakula majani na viumbe wenye sumu kama washawasha au viwavi wa baharini (jerry fish) hivyo kuwafanya kuwa na sumu.

“Faida kubwa ya uwepo kwa kasa ni chanzo cha kuongezeka kwa samaki baharini kwa sababu ile mimea na wanyama wenye sumu ikiongezeka samaki hukimbia hivyo uwepo wa kasa baharini husaidia kuongezeka kwa samaki”amesema Mapoy

Mapoy amefafanua kuwa hata binadamu akiguswa na viwavi hao (jerry fish) huwashwa mwili na huweza kusababisha kifo.

“Kasa ni moja ya kiumbe aliye hatarini kutoweka kutokana na kuliwa na binadamu ambapo kundi lao linawajumuisha Nguva,Papa Potwe,Pomboo na Nyangumi hawa wote wapo hatarini kutokweka

Aklizungumzia kuhusu sheria,Mapoy anabainisha kuwa sheria zipo na ni kali ambapo  hupelekea mtu kutumikia kifungo cha miaka 10 gerezani ikiwa atakutwa na hatia.

Next Post
Kasa ‘Daktari wa bahari’ aliye hatarini kutoweka

Kasa 'Daktari wa bahari' aliye hatarini kutoweka

MISA-TAN yataka marekebisho sharia ya habari

MISA-TAN yaomba marekebisho sheria huduma za habari

Bonde la Mto Kilombero hatarini

Bonde la Mto Kilombero hatarini

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In