NA MWANDISHI WETU
SHUGHULI za binadamu katika miji ya Lupilo,Ifakara na Mlimba zimesababisha kuchafuliwa kwa Bonde la Mto Kilombero kwa asilimia 80 na taka ngumu.
Bonde hilo ambalo ni maarufu kwa kilimo cha mpunga na shughuli za uvivi wa samaki linatajwa kuwa ndio eneo la kimkakati katika uzalishaji wa chakula nchini.
Kwa mujibu wa Ripoti ya Jumla ya Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Charles Kichere katika Ukaguzi wa Ufanisi kwa kipindi kinachoishia Machi 31, 2022 juu ya udhibiti usiojitosheleza wa uchafuzi ndani ya Mifumo ya Ardhioevu.
Amesema ukaguzi ulibaini kwamba Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA), Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), na Halmashauri hazikudhibiti ipasavyo uchafuzi wa mazingira katika mifumo ya ikolojia ya ardhioevu.
Amesema hilo lilithibitishwa na uwapo wa uchafuzi kutokana na taka ngumu katika maeneo ya ardhioevu manne kati ya nane yaliyotembelewa, ambapo uchafuzi kutokana na taka ngumu ulikuwa kati ya asilimia 0 hadi 80.
Ripoti hiyo ya CAG imefafanuwa kuwa Eneo la Ardhioevu la Bonde la Mto Kilombero lilikiwa na uchafuzi wa juu wa asilimia 80.
“Sababu ya Bonde la Mto Kilombero kuwa na uchafuzi wa kiwango cha juu zaidi kutokana na taka ngumu ni uwapo wa maendeleo ya shughuli za kibinadamu katika Miji ya Ifakara, Mlimba na Lupilo.
“Ukaguzi ulibaini kuwapo kwa uchafuzi kwa majitaka katika maeneo ya ardhioevu yaliyotembelewa ambapo maeneo matano kati ya nane yaliyotembelewa yalionesha uwapo wa uchafuzi wa majitaka.
“Ukaguzi ulibaini kuwa, shughuli za kibinadamu zilichangia kuzuka kwa tatizo la mmomonyoko na kujaa kwa udongo kwenye maziwa na mito kama vile Ziwa Sagara, Ziwa Nyamagoma, Mto Malagarasi, pamoja na kwenye vyanzo vingine vya maji imeongeza ripoti hiyo.
mwisho




Discussion about this post