• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Waharibu saruji kupinga mradi wa maji

by bajeti
July 1, 2022
in Habari
0
Waharibu saruji kupinga mradi wa maji

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, wananchi wa Kijiji cha Bucha wilayani Babati Mkoa wa Arusha wameharibu mifuko 60 ya saruji kupinga mradi wa maji katika kijiji chao.

Wananchi hao mbali na kuharibu mifuko hiyo lakini pia waliharibu jengo lililotumika kuhifadhia vifaa na kuviharibu.

Hayo yamebainishwa na Ripoti  ya  Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), Charles Kichere  kuhusu Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2020/21.

Katika ripoti hiyo ilifafanua kuwa vurugu hizo za wananchi zilisababisha  Mradi wa Maji wenye thamani ya Sh. Bilioni 7.49 kuchekelewa kutokana na vurugu zilizofanywa na wananchi wa eneo hilo kufuatia tangazo la Serikali lililotolewa  Septemba 6,2019, Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dareda (Dareda WSSA) ilivunjwa na Waziri na kukabidhi majukumu yake kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA).

 

Ripoti hiyo iliongeza kuwa kabla ya hapo, Dareda WSSA ilikuwa ikitekeleza mradi wa usambazaji wa maji wa Dareda – Singu – Sigino na Bagara ambapo chanzo cha maji kilikuwa katika kijiji cha Bacho ambapo gharama zote za mradi zilikadiriwa kuwa Sh. bilioni 7.49 ambao ulianza Februari mosi, 2020 na ulitarajiwa kukamilika Desemba 31, 2021 huku mradi huo ulishapokea jumla ya Sh.Milioni 400 na ulikuwa umetumia Sh.Milioni 105.3.

“Kabla ya BAWASA kuanza utekelezaji wa mradi huo, ilikumbana na vikwazo kutoka kwa wananchi kutokana na wanakijiji kukataa mradi huo.

“Pia, waliharibu jengo la kuhifadhia vifaa na kuharibu vifaa vya mradi (mifuko ya saruji 60 na vyuma vilivyotakiwa kutumika kwenye mradi) vyenye thamani ya Sh. Milioni 3.052 vilivyonunuliwa kwa ajili ya ujenzi wa chanzo cha maji katika kijiji cha Bacho.

Hata hivyo ripoti hiyo ilibainisha kuwa kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mradi ya  Agosti 30, 2021, kukamilika kwa mradi kulikuwa ni  asilimia 10 tu, kinyume na matakwa ya Kanuni Na. 114 ya Kanuni za Ununuzi wa Umma ya mwaka 2013 ambayo inaitaka taasisi nunuzi kuwajibika katika usimamizi madhubuti ya ununuzi wowote wa bidhaa, huduma au kazi inazozifanyia.

“Hivyo mradi ulichelewa kutokana na vurugu zilizosababishwa na jamii kutoshirikishwa ipasavyo wakati wa uanzishaji wa mradi.

“Nina mashaka na kipindi kilichosalia hadi tarehe mradi unapotarajiwa kukamilika, yaani Desemba 31,2021. Hivyo, mradi uko katika hatari ya kutokamilika kwa muda uliopangwa”ilifafanua ripoti hiyo

Kutekeleza mradi kunasababisha kuongezeka kwa gharama na hivyo inapunguza juhudi za Serikali kuhakikisha upatikanaji wa maji safi kwa jamii.

 

“Ninashauri menejimenti ya Wizara ya Maji kwa kushirikiana na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA) na Mamlaka za Mikoa ili kutatua migogoro na jamii inayowazunguka kwa kuishirikisha jamii ipasavyo ili kujenga umiliki wa mradi kwa jamii kwa maendeleo endelevu ya mradi.

“ Kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi wa Dareda-SinguSigino ili kuwezesha utoaji wa huduma ya maji kwa jamii.”ilibainisha ripoti hiyo

mwisho

Next Post
WHO:Bidhaa za tumbaku zina kemikali zaidi ya 7000 za sumu

WHO:Bidhaa za tumbaku zina kemikali zaidi ya 7000 za sumu

Vikombe vya plastiki vyapigwa marufuku

Vikombe vya plastiki vyapigwa marufuku

Zambia kujenga bomba la kisasa kusafirisha mafuta

Zambia kujenga bomba la kisasa kusafirisha mafuta

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:17
  • Today's page views 17
  • Total visitors 13,276
  • Total page views 15,024

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In