• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Vikombe vya plastiki vyapigwa marufuku

by bajeti
July 5, 2022
in Mazingira
0
Vikombe vya plastiki vyapigwa marufuku

Vikombe na vyombo vingine vya plastiki

Share on FacebookShare on Twitter

NEW DELHI,INDIA

INDIA imepiga marufuku matumizi vikombe vya plastiki ikiwemo kutupwa bidhaa zingine za plastiki kama sehemu ya mpango wa kulinda mazingira.

India yenye watu zaidi ya Bilioni 1.4 imebainisha vitu 19 vya plastiki ambavyo havina umuhimu sana lakini vinaweza kuwa takataka, hivyo kupekelea kusitisha uzalishaji, uagizwaji, usambazaji na uuzaji.

Vitu hivyo ikiwemo vikombe vya plastiki na vijiti vya ice cream pamoja na baadhi ya mifuko ya plastiki itasitishwa na kutakuwepo na mifuko mbadala.

Maelfu ya bidhaa zingine za plastiki  kama chupa za maji, soda na mifuko ya chakula, haijajumuishwa kwenye katazo hilo.

Lakini Serikali imeweka malengo kwa wazalishaji kuvichakata tena au kuvitupa baada ya kuvitumia.

Akizungumza na waandishi wa habari nchini humo Waziri wa Mazingira wan chi hiyo  Bhupender Yadav amesema marufuku hiyo ilikuwa imetangazwa kwa mwaka mmoja ambapo sasa muda umekwisha.

Kwa upande wake Mratibu wa Kikundi cha Asia-Pasific  Satyarupa Shekhar alisema marufuku hiyo ya nchi nzima inajumuisha sio matumizi ya plastiki lakini pia uzalishaji au uagizaji wake

Hata hivyo watengenezaji wa plastiki waliiomba serikali ya nchi hiyo kuchelewesha katazo hilo, kutokana na mfumuko wa bei na upotezaji wa ajira utakaotokea.

Mamilioni ya tani za taka hizo za plastiki huchafua bahari  na huathiri wanyamapori ambapo wanasayansi bado wanajaribu kutathmini hatari zinazosababishwa na vipande vidogo vya plastiki .

Utengenezaji wa plastiki hutoa gesi chafu zinazo ongeza joto duniani ambapo  India ni nchi yenye viwanda vinavyotengeneza zaidi ya tani 243,000 za taka za plastiki kila mwaka.

Utafiti hivi karibuni,umeonesha kuwa zaidi ya viungio vya kemikali 8,000 vinatumika kwenye usindikaji wa plastiki, na hutoa gesi chafu.

mwisho

Next Post
Zambia kujenga bomba la kisasa kusafirisha mafuta

Zambia kujenga bomba la kisasa kusafirisha mafuta

Maendeleo Sekta ya Gesi na Mafuta kusaidia miradi ya kimkakati

Maendeleo Sekta ya Gesi na Mafuta kusaidia miradi ya kimkakati

SMT:Ukosefu wa nidhamu unasababisha miradi kutokalimika

SMT:Ukosefu wa nidhamu unasababisha miradi kutokalimika

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:17
  • Today's page views 17
  • Total visitors 13,276
  • Total page views 15,024

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In