• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali yaandaa mpango-kazi kuondoa matumizi ya Zebaki

by bajeti
November 14, 2021
in Mazingira
0
Serikali  yaandaa mpango-kazi kuondoa matumizi  ya  Zebaki
Share on FacebookShare on Twitter
Mmoja wa wachimbaji wadogo wa dhahabu kutoka Mgodi wa Chikoa uliopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma ambaye jina lake halikufahamika akitoa maelezo kwa waandishi wa habari waliotembelea mgodi huo hivi karibuni jinsi wanavyotumia kemikali ya Zebaki katika kuchenjulia dhahabu (Picha na mpigapicha wetu)

SERIKALI imeandaa Mpango-Kazi wa Taifa wa Kupunguza Matumizi ya kemikali aina ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu  ili kulinda afya za wananchi,viumbe hai na mazingira.

Kemikali hiyo hatari inadaiwa kuharibu ubongo na mfumo wa mishipa ya fahamu, figo,kuzaliwa watoto wenye ulemavu,kupoteza kumbukumbu ikiwemo kushindwa kupumua imekuwa ikiingizwa kwa kificho ambapo watumiaji wakubwa ni wachimbaji wadogo wanayoitumia bila kufuata utaratibu wake.

Mpango-Kazi huo wa mwaka 2020-2025 umekuja ili kukidhi matakwa ya Mkataba wa MINAMATA ukiwa na lengo la kupunguza matumizi ya Zebaki ikiwezekana kuiondosha kemikali hiyo katika shughuli za wachimbaji wadogo wa dhahabu na kutumia teknolojia mbadala.

Akizungumza katika semina ya waadishi wa habari jijini Dodoma,Mkurugezi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dk.Andrew  Komba amesema Zebaki ni kemikali hatari kwa mazingira na viumbe hai na madhara yake ni ya muda mrefu.

“MINAMATA ni moja ya Jimbo lililoko nchini Japan ambalo kulikuwa na kiwanda cha kutengeneza kemikali mbalimbali na kiliajiri wakazi wengi wa eneo hilo na kemikali iliyokuwa ikitumika sana ni Zebaki.

“Maji yake yalikuwa wakimwagwa baharini na shughuli kuu katika eneo hilo ni uvuvi hivyo tangu miaka ya 1930 athari zake zinaonekana hadi sasa na mimi nilienda huko mwaka 2018 athari zake ni kubwa hivyo lazima waandishi msaidie kuelimisha umm”amesema Dk Komba

Dk Komba amefafanua kuwa serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kukabiliana na kemikali hiyo ikiwemo kutafuta teknolojia mbadala itakayoweza kutumika na wachimbaji wadogo ili kuepusha madhara makubwa kwa jamii.

Baadhi ya Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini na wachimbaji wadogo wa dhababu, wakimsikiliza Meneja wa Mgodi wa Chikoa uliopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma Zebedayo Matunde wakati akitoa maelezo jinsi matumizi ya kemikali ya zebaki inavyotumika katika kuchenjulia madini kulingana na miongozo iliyowekwa na serikali (Picha na mpigapicha wetu)

Kwa upande wake  Mhandisi Kamukuru Maganya kutoka  Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira amesema Zebaki inayotumika katika shughuli za wachimbaji wadogo hapa nchini huingizwa kutoka nje ya nchi kupitia njia zisizo rasmi na huonekana katika matumizi pekee.

“Ni lazima uingizwaji,uhifadhi,matumizi yake ya Zebaki  yafuate utaratibu maalum kwani hadi sasa kuna wachimbaji wadogo zaidi ya milioni 1.2 na wote hawa wanatumia kemikali ya zebaki kupata dhahabu”amesema  Maganya

Kwa upande wake Abel Madaha kutoka Tume ya Madini amesema kemikali hiyo inapobaki katika ardhi hubadilika na kuwa sumu hivyo serikali iliamua kuweka Sheria na Kanuni juu ya Zebaki na kemikali nyingine ili kuweza kudhibitiwa.

“Serikali imehakikisha inajenga vituo maalum  vya uchenjuaji wa dhahabu,kutoa mafunzo na semina mbalimbali kwa wachimbaji wadogo ambao ndio waathirika wakubwa katika matumizi ya kemikali hiyo na kuhakikisha kuwa wanavaa vifaa kinga wakati wa uchenjuaji wa dhahabu”amesema Madaha

Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira (JET) John Chikomo amebainisha kuwa ni wajibu wa waandishi wa habari kuisaidi serikali katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa sahihi za mazingira kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Andrew Komba akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Mpango-Kazi wa Kupunguza Matumizi ya kemikali ya Zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu (2020 -2025), jijini Dodoma jana.Kushoto ni Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET) John Chikomo na Ofisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhandisi Kamukuru Maganya

Oktoba 9,2013,Serikali kutoka nchi mbalimbali duniani zilianza kutia saini Mkataba wa Kuzuia Matumizi ya Zebaki baada ya mashauriano ya miaka minne .

Mkataba huo unaweka uthibiti na upunguzaji wa matumizi ya madini hayo ya Zebaki katika vifaa tiba na kwenye sekta ya uchimbaji madini na viwanda vya saruji. Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Mazingira (UNEP) limefafanuwa kuwa madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya Zebaki ni pamoja na kuharibu ubongo na mfumo wa mishipa ya fahamu

Next Post
Serikali  yaandaa mpango-kazi kuondoa matumizi  ya  Zebaki

Tani 24 za zebaki hutumika kuchenjulia dhahabu

SMT:Mshirikiane na serikali  kuzuia uharibifu wa mazingira

SMT:Mshirikiane na serikali  kuzuia uharibifu wa mazingira

Majengo kuwekewa mfumo wa umeme kuchajisha magari

Majengo kuwekewa mfumo wa umeme kuchajisha magari

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In