• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

SOS Children’s Villages yapongezwa kusaidia uanzishwaji UWAMTO

by bajeti
August 1, 2022
in Habari
0
SOS  Children’s Villages yapongezwa kusaidia uanzishwaji UWAMTO

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Daud Mpoli akizungumza na viongozi wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha vilivyo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Children's Village vinavyounda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO) unaohusisha Kata za Chanika na Zingiziwa juu ya changamoto zinazojitokeza ili kuuendeleza mfuko huo(Picha na Goodluck Hongo)

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU

AFISA Maendeleo ya Jamii kutoka Jiji la Dar es Salaam Daudi Mpoli ameishukuru  SOS Children’s Villages  katika kusaidia kuondoa ukatili dhidi ya mtoto katika  ngazi ya Kata,Wilaya,Mkoa,na Wizara.

Mpoli amebainisha kuwa SOS Children’s Villages imefanya kazi kubwa katika ngazi mbalimbali za  Wizara,Mkoa,Wilaya na Kata na kuwataka wale wote wanaowezeshwa kuendeleza miradi hiyo ili iwe endelevu.

Mpoli ametoa kauli  hiyo leo Chanika jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha zaidi ya 30 vinavyo jishughulisha na masuala ya kupinga ukatili kwa mtoto.

Vikundi hivyo ambavyo vipo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Childrens Village unahusisha  Kata za Chanika na Zingiziwa zilizopo Jiji la Dar es Salaam ambapo pia vimefanikiwa  kuunda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO)

Akizungumza na viongozi wa vikundi hivyo,Mpoli amefafanuwa kuwa   ipo siku SOS Children’s Villages itaondoka lakini jamii itaendelea kuwepo hivyo ni lazima kuwa na mifumo endelevu ya miradi na kazi zinazotolewa na SOS Childrens Village.

“Nawapongeza sana juu ya kufanikiwa kuanzisha mfuko huu wa watoto katika Kata za Zingiziwa na Chanika lakini lazima mfanye kazi kisasa kwa kushirikiana na serikali kwani watu wanaopata mahitaji kutokana  taasisi mbalimbali wapo wengi lakini Balozi na Afisa Maendeleo wa Kata wanajua taasisi na idadi ya watoto wanaosaidiwa katika eneo husika.

“Sisi kama serikali mikopo ipo katika vikundi kama hivi ili kutunisha mfuko huo kwani kutokana na Rais Samia Suluhu Hassan kuweka mfumo bora kwa vikundi kupata mikopo  bila mlolongo”amesema Mpoli

 

Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Jiji la Dar es Salaam Daud Mpoli akiwaonesha viongozi wa vikundi vya huduma ndogo za kifedha vilivyopo chini ya Mradi wa Kuimarisha Familia na Ustawi wa Mtoto kutoka SOS Children’s Village na kuunda Umoja wa Usimamizi wa Mfuko wa Mtoto (UWAMTO) katika Kata za Chanika na Zingiziwa jijini Dar es Salaam leo jinsi kutatuta na kuendeleza mradi huo(Picha na Goodluck Hongo)

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Development Concern linalofanyakazi kwa kushirikiana na SOS Children’s Villages (DECO) Robert Nyampiga amesema wamekutana na vikundi hivyo ili kutoa mwongozo  na kutatua changamoto zinazohusina na uendeshaji wa mfumo huo wa UWAMTO.

Amesema SOS Children’s Villages ni mwezeshaji na melezi wa vikundi  32 na wao kama DECO ni wawezeshaji  ambapo vikundi hivyo licha ya kuwezeshwa kufanya masuala ya ujasiriamali ili kujiongezea kipato lakini pia kuendelea na shughuli za kupinga ukatili dhidi ya mtoto.

Nyampiga amebainisha kuwa mradi huo ulianza baada ya SOS Children’s Villages   kuona ongezeko kubwa la ukatili dhidi ya watoto hivyo kuamua kuuanzisha ambapo  umesaidia kupunguza vitendo hivyo kwa asilimia 80 katika Kata hizo.

Naye Mwenyekiti wa UWAMTO Shirazi Sinde  amesema changamoto waliyonayo kwa sasa ni uendelewa mdogo kwa wananchi juu ya UWAMTO kwa kuwa wao kama jamii wamekuwa wakisaidia watoto pindi wanapofanyiwa ukatili.

Mwakilishi wa Kikundi cha Tuwezeshane Maonesho Rashidi amesema   SOS Children’s Villages wamefanya kazi kubwa ikiwemo kuchimba visima,kujenga madarasa na kusaidia watoto hasa katika kuibua ukatili dhidi ya watoto.

“Serikali inahuruma lakini tungeomba SOS Children’s Villages wasimamie wenyewe ikiwemo kusimama mahakamani kutoa ushahidi maana kazi waliyoifanya imesaidia sana kupungua kwa vitendo vya ukatili kwa watoto katika eneo hili tofauti na ziku za nyuma”amesema Maonesho

Next Post
Majaliwa:Viongozi fuateni falsafa ya Serikali kuhudumia wananchi

Majaliwa:Viongozi fuateni falsafa ya Serikali kuhudumia wananchi

Dkt.Chana:Maliasili  yatengewa bajeti zaidi ya Sh.Bilioni 600

Dkt.Chana:Maliasili yatengewa bajeti zaidi ya Sh.Bilioni 600

Mkandarasi apewa siku 14 kukamilisha mradi EBARR

Mkandarasi apewa siku 14 kukamilisha mradi EBARR

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:8
  • Today's page views 8
  • Total visitors 13,064
  • Total page views 14,809

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In