• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali yakitaka Kiwanda cha A to Z kukamilisha mtambo wa kutibu majitaka

by bajeti
September 21, 2022
in Mazingira
0
Serikali yakitaka Kiwanda cha A to Z kukamilisha mtambo wa kutibu majitaka

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)(aliyenyoosha mkono) Khamis Hamza Khamis akitoa maelekezo kwa viongozi wa Kiwanda cha nguo cha A to Z kuhusu kukamilishwa kwa mtambo wa kutibu majitaka wakati alipotembelea kiwanda hicho kukagua maagizo ya serikali Septemba 21,2022.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,ARUSHA

NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis amekitaka kiwanda cha nguo cha A to Z kilichpo mkoani Arusha kikamilishe ujenzi wa mtambo wa kutibu majitaka ndani ya miezi miwili.

Khamis ametoa maelekezo hayo Septemba 20,2022 jijini Arusha wakati alipofanya ziara ya kukagua na kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu kuondoa changamoto ya harufu na majitaka yanayotirirka kupita mtaro unaopita kwenye makazi ya watu.

Hata hivyo Khamis ameelekeza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Kaskazini, wataalamu wa mazingira kutoka Ofisi za Mkuu wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri ya Jiji la Arusha kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha maeleekzo hayo yanatekelezwa.

“Hamuwezi kujua hizi harufu mbaya za haya majitaka yanayotoka hapa na kutiririka kwenye makazi ya watu zina athari gani, sasa ninatoa miezi miwili mkamilishe mtambo wa huu,” amesema Khamis.

Aidha,Khamis amebainisha kuwa  kiwanda hicho kimekuwa kikilamikiwa na wanachi kwa muda mrefu kwa uchafuzi wa mazingira kwa kutiririsha majitaka katika makazi ya wananchi.

Amesema Serikali inawapenda wawekezaji lakini wakati huohuo inalinda afya za wananchi wake pamoja na hifadhi ya mazingira lakini kiwanda hicho kimekuwa kikilamikiwa na wananchi kuhusu kuchafua mazingira.

Awali Meneja wa NEMC Kanda ya Kaskazini Lewis Nzali amesema baraza hilo limekuwa likitoa maelekezo mbalimbali ikiwemo kukipiga kiwanda hicho faini kwa uharibifu wa mazingira.

Nzali amebainisha kuwa kutokana na hatua hizo kiwanda cha A to Z kimeweza kuanza kujenga mtambo wa kuchakata majitaka kabla ya kwenda kwenye mazingira.

Nzali ameongeza kuwa hatua hiyo imeleta mafanikio katika sekta ya uwekezaji nchini kwa kuweza kuzingatia Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004.

Kwa upande wake Meneja wa Kiwanda cha A to Z  Sylivester Kazi ameahidi kukamilika kwa ujenzi wa mtambo huo ili kulinda afya za wananchi wanaozunguka eneo hilo.

Mtambo huo umegharimu kiasi cha sh. Bilioni moja ambapo kukamilika kwake kutaondoa tatizo la majitaka kutiririka katika makazi ya wanachi na kusambaa kwa harufu mbaya.

 

Next Post
Vyombo vya habari vyaombwa  kuandika habari za Kanisa

Vyombo vya habari vyaombwa kuandika habari za Kanisa

Mchanga;rasilimali ya pili kutumika duniani baada ya maji

Mchanga;rasilimali ya pili kutumika duniani baada ya maji

Tanzania yashiriki Kombe la Dunia kwa Watu wenye Ulemavu.

Tanzania yashiriki Kombe la Dunia kwa Watu wenye Ulemavu.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In