NA GOODLUCK HONGO
ZAIDI ya makanisa 10 jijini Arusha wameunga mkono juhudi za Mch. Daudi Mashimo za kumpongeza Nabii Mkuu Dkt, GeorDavie wa Kanisa la GeorDavie Ministries International (Ngurumo ya Upako) kupitia matembezi yaliyopewa jina la Ngurumo ya Upako Matembezi Marathoni.
Matembezi hayo yaliyofanyika Oktoba mosi,2022 jijini Arusha kutokana na Kiongozi huyo kusaidia jamii kwa hali na mali ikiwemo kutoa fedha taslimu.
Mbali na kutoa fedha na magari kwa nyakati tofauti lakini pia amekuwa akiguswa na hali waliyonayo baadhi ya waumini wake na wasio waumini wake hivyo kuamua kuwasaidia kwa kuwapatia mitaji zikiwemo fedha taslimu.
Matembezi hayo yaliyopewa jina la Ngurumo ya Upako Matembezi Marathoni yaliwajumuisha watu mbalimbali walioguswa na matukio ya kujitoa kwa kiongozi huyo kwa jamii na wengine waliofanikiwa kujikwamua kiuchumi kutokana na misaada ya Nabii huyo.
Kiongozi huyo wa Kanisa mbali na kusaidia jamii lakini pia amekuwa akiunga mkono juhudu za serikali pindi wanapohitaji msaada kutoka kwake.
Baadhi ya taasisi za serikali ambazo zimefaidika na msaada huo ni pamoja na Jeshi la Magereza Mkoa wa Arusha ambapo lilipokea Sh.Milioni 20 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi katika maeneo ya gereza.
Hata hivyo baadhi ya vyama vya siasa navyo havikuachwa katika kupata msaada wa Kanisa hilo la Ngurumo ya Upako.
Nabii Mkuu Dkt.GeorDavie amekuwa akizungumza ndani ya Kanisa lake lililopo Kisongo jijini Arusha sababu za kutoa misaada hiyo ya kifedha,vyombo vya moto kama magari,pikipiki za magurudumu matatu na misaada mingine ikiwemo kusaidia vituo vya kulelea watoto yatima.
“ Mimi naona ni jambo zuri na la baraka kwa kufanya hivi hasa tunapokuwa tumefanikiwa katika maisha ni vizuri tuwakumbuke watu wadogo tukijua ndiko tulikotoka,na watu wenye uwezo wawakumbuke watu wadogo.
“Watu wadogo kwa kweli ni watu wanafanya kazi mchana na usiku ndio wanajitahidi,ndio wanabeba Taifa hili kwa asilimia kubwa sana,kwa hiyo tuwakumbuke vijana wetu wadogo wainuke”
Kauli hiyo ya Nabii Mkuu Dkt.GeorDavie aliitoa jijini Arusha wakati akitoa fedha zaidi ya Sh.Milioni 10 kwa wafanyabiashara wa Soko la Kisongo wakati alipofanya ziara ya kuwatembelea.
Oktoba mosi ,2022,Makanisa zaidi ya 10 yalishiriki katika kuandaa matembezi ya kumpongeza Kiongozi huyo kutokana na kusaidia jamii bila ubaguzi.
Katika matembezi ya marathon hiyo yaliyohudhuriwa na waumini wa makanisa mbalimbali ikiwemo wasanii na watangazaji wa vituo vya redio nchini lilionesha jinsi kiongozi huyo anavyodhamini maisha ya walio katika hali ya chini na kuwainua kuichumi.
Akizungumzia kuhusu sababu za pongezi hizo kupitia matembezi,mmoja wa waandaaji wa matembezi haye Mchungaji David Mashimo amesema sababu kubwa ya kuandaa ni kuguswa na misaada yake kwa jamii bila ubaguzi.
Mashimo amebainisha kuwa wametumia zaidi ya Sh.Milioni 18 kuandaa tamasha hilo ambalo lilihudhuriwa na mamia ya watu wa Jiji la Arusha na mikoa jirani.
“Haya ni matembezi ya pili, ya kwanza tulifanya Dar es Salaam na kutembea kilomita zaidi ya 15 kwa ajili ya kumpongeza na ya pili ni haya ya Oktoba Mosi,2022 hapa katika viwanja vya Mgambo jijini Arusha ili kuendelea kumpongeza”amesema Mashimo




Discussion about this post