• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Prof.Tibaijuka ataka wazazi kuwalinda watoto dhidi ya mitandao ya kijamii

by bajeti
October 16, 2022
in Habari
0
Prof.Tibaijuka ataka wazazi kuwalinda watoto dhidi ya mitandao ya kijamii

Waziri wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof.Anna Tibaijuka akimkabidhi zawadi ya cheti mwanafunzi wa Shule ya Mother of Mercy John Mlyambina jijini Dar es Salaam jana wakati wa mahafali ya saba ya shule hiyo.Katikati ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Fredinand Ilungu.(Picha na mpigapicha wetu.)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof.Anna Tibaijuka amewataka wazazi nchini kuwa makini na mitandao ya kijamii katika malezi ya watoto wao.

Amesema katika wakati huu wa utandawazi  na kukuwa kwa technoljia duniani inayoifanya kuwa kijiji kimoja kuna mianya mingi ya kuporomosha maadili ya mila na desturi na hasa vijana wa kati ya umri wa miaka 15 hadi 25.

Prof.Tibaijuka ametoa onyo hilo Oktoba 15,2022  jijini Dar es Salaam  wakati akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi wa Shule ya Mother of Mercy katika mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo.

Amesema kundi hilo la watoto ndio linaloathirika zaidi na mitandao ya kijamii hivyo ni muhimu kwa wazazi kukaa mbali na watoto pindi wanapotumia akaunti  za mitandao yao.

“Ni lazima kuwa makini na hili na usiwaachie wajifunze vitu ambavyo wewe hujui, ni vema ukavijua na ukaweza kumpa mwanao tahadhari kwa jambo husika”amesema Tibaijuka

Tibaijuka ameongeza kuwa licha ya umuhimu wa mitandao kuwa na fuksa za ajira,elimu na biashara ya kwa watu wenye umri mkubwa zaidi lakini kwa watoto ni muhimu ikajulikana   anatumia kwa malengo ya kuelimika na si vinginevyo.

Waziri wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof.Anna Tibaijuka (wa pili kulia), akikata keki na Mkurugenzi wa Shule ya Mother of Mercy Regina Rwegasira, (kulia) wakati wa mahafali ya darasa la saba ya shule hiyo yaliyofanyika Madale-Kinondoni jijini Dar es Salaam jana.Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Fredinand Ilungu na Ofisa Elimu Manispaa ya Kinondoni Theresia Kyara.(picha na mpigapisha picha wetu

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Shule hiyo  Regina Rwegasira amesema licha ya kufundisha lakini pia kipaumbele chao kingine ni nidhamu kuanzia wanafunzi,walimu hadi wafanyakazi wa shule.

“Shule haiwezi kumvumilia mwalimu au mtumishi anayekiuka maadili lakini pia tunafundisha watoto kumjua mungu kwa kila mwanafunzi na imani yake ya dini ili kuwa watoto bora wanapokwenda katika jamii”amesema Rwegasira

Hata hivyo Rwegasira amefafanuwa  kuwa licha ya mtoto kumaliza katika shule yao lakini wana mfumo wa kuwafuatili huko wanakokwenda ili kuwasaidia zaidi kitaaluma ili kuwa na kizazi bora kwa Taifa.

Shule  ya Mother of Mercy imejipatia  umaarufu kwa kutoshuka nafasi ya 10 bora katika maotokeo ya Mkoa Dar es Salaam na kushika nafsi za juu kwa mitihani ya kitaifa.

Waziri wa zamani wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof.Anna Tibaijuka akimlisha keki mhitimu wa darasa la saba katika Shule ya Mother of Mercy Maida Ismail wakati wa mahafali ya saba ya shule hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.Kulia ni Ofisa mwandamizi wa shule hiyo Lilian Mbelwa.(Picha na mpigapicha wetu)

 

 

 

Next Post
Kanda ya Ziwa kunufaika na miradi ya kimkakati

Kanda ya Ziwa kunufaika na miradi ya kimkakati

Majaliwa:Viongozi fuateni falsafa ya Serikali kuhudumia wananchi

Majaliwa ampa siku 15 mkandarasi kukamilisha miradi ya barabara

Serikali yawaonya Wakadiriaji Thamani za Ardhi na Mali

Serikali yawaonya Wakadiriaji Thamani za Ardhi na Mali

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In