MWENYEKITI wa Taasisi ya isiyo ya Kiserika ya Jai Juma Mwipopo amesema wataendelea kusaidia makundi mbalimbali ya jamii wasiojiweza ili kuwafariji kutokana na hali ngumu wanayopitia.
Mwaipopo ametoa kauli hiyo leo Oktoba 30,2022 jijini Dar es Salaam siku moja baada ya kukabishi misaada katika gereza la Segerea
Mwaipopo ambaye ni Diwani Mstaafu wa Kata ya Jimbo la Ukonga amesema wameshatembelea na kutoa misaada kwa akinamama wajane,wazee,wagonjwa na wengine wanaohitaji msaada kutokana na kuwa na hali ngumu ya kiuchumi.
“Sisi kama Jai ni wajibu wetu kutoa misaada ya vyakula,nguo,sabuni na hata wakati mwingine kuchangia matibabu kidogo ya wagonjwa ikiwemo damu ili kuwafariji wenzetu kwa kuwa ni lazima tuishi kama ndugu hivyo kusadia wasiojiweza ni baraka pia”amesema Mwaipopo
Mwaipopo amebainisha kuwa mbali na kutoa misaada hiyo kwa jamii lakini pia hawajawasahau watu walioko gerezani ambao kwa wakati na wao wanahitaji msaada hata kama ni kidogo.
Taasisi hiyo tayari imeshatoa misaada mbalimbali kwa makundi tofauti wakiwemo wajane katika Jimbo la Ukonga na kusaidia baadhi ya wajasiriamali kupata mikopo na wengine kutoa ajira zaidi baada ya kupata mafunzo ya ujasiriamali.
“Pamoja na kwamba tunawakumbuka walioko gerezani lakini pia huwa tunahamasisha watu wachangie damu ili kusaidia wagonjwa wanaojitaji kusaidiwa “ameongeza Mwaipopo




Discussion about this post