NA MWANDISHI WETU
MAKAMU wa Rais Dkt.Philip Mpango amewasili jijini Abidjan nchini Ivory Coast ambapo atamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa la Uwekezaji Barani Afrika litakalofanyika Novemba 2-4. 2022.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Oktoba 31,2022 kwa vyombo vya habari na Msaidizi wa Makamu wa Rais – Habari Franco Singaile amesema Makamu wa Rais amewasili nchini humo Oktoba 31,2022.
Amesema akiwa nchini humo anatarajia kuongoza mazungumzo baina ya Tanzania na wawekezaji mbalimbali kuhusu uwekezaji katika miradi ya kimkakati nchini Tanzania katika Sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji, Usafirishaji na Uchukuzi.
Amesema Jukwaa la Uwekezaji Barani Afrika linaratibiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa kushirikiana na waanzilishi wa Jukwaa hilo na linalenga kuwakutanisha Wawekezaji, Sekta Binafsi na Sekta ya Umma ili kuweka mikakati ya kufadhili miradi endelevu.
Aidha amebainisha kuwa Jukwaa hilo linashirikisha Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika, Wakuu wa taasisi na mashirika ya kimataifa pamoja na wafanyabiashara.




Discussion about this post