NA MWANDISHI WETU,DODOMA
WAZIRI wa Nchi Osi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo amepokea taarifa fupi ya usashaji wa Mto Msimbazi kutokana na maelekezo aliyotoa hivi karibuni kwa Kikosi cha Kuratibu Usashaji Mito na Mabonde Mkoa wa Dar es Salaam.
Taarifa hiyo imewasilishwa kwa Waziri Jafo osini kwake jijini Dodoma leo Novemba mosi,2022 ,na Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha kuratibu usashaji wa Mito na Mabonde Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Elizabeth Mshote.
Hivi karibuni alifanya ziara ya kikazi ya kukagua mto huo katika Kata ya Mogo Mtaa wa Kipawa baada ya kupokea malalamiko kuhusiana na athari za kimazingira zinazotokana na usashaji wa mto huo.
Hata hivyo, wakati wa ziara hiyo baada ya kusikiliza maoni ya wananchi alipata maoni yanayokinzana ambapo wengine walidai shughuli za usashaji mto huo zimeleta athari kwa mazingira na wengine wakidai zimeleta manufaa makubwa kwa jamii inayozunguka eneo hilo.
Itakumbukwa Februari 2021 Waziri Jafo alikutana na wadau wanaojishughulisha na uchimbaji mchanga katika mkoa huo kujadili changamoto za kimazingira zinazotokana na uchimbaji mchanga kiholela kiholela katika mito na mabonde ili kuweka utaratibu mzuri.

Waziri wa Nchi Osi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira)
Dkt. Selemani Jafo leo Novemba Mosi,2022, akipokea taarifa ya Usashaji wa Mto
Msimbazi kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikosi kazi cha Kuratibu Usashaji
wa Mito na Mabonde Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Elizabeth Mshote
alipoiwasilisha ofisini jijini Dodoma.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira)
Kikao hicho kiliwezesha kuandaliwa Mwongozo wa usashaji mito utakaotumika katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuondoa mchanga, taka ngumu na tope ili kupunguza au kuondoa madhara ya mafuriko ambao ulitolewa kwa mujibu wa kifungu cha 57 (2) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004.




Discussion about this post